Hakimu atoa onyo kesi vigogo Rahaco...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
Abdulrahim Sadiki
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa onyo la kuifuta kesi ya kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani 527,540, inayowakabili vigogo wa kampuni
hodhi ya mali za reli (Rahaco) kwa kiwango ambacho washtakiwa hao hawatakamatwa
tena.
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba ametoa
onyo hilo baada ya ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka (DPP) kuomba siku 14 ili
kukamilisha utaratibu wa kupeleka taarifa za kesi hiyo, Mahakama Kuu.
Ombi
hilo lilitolewa jana na mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na
rushwa(Takukuru), Mghela Ndimbo
Kufuatia
maelezo hayo, Hakimu Simba alitoa
ahirisho la mwisho na kuwaeleza kuwa ataifuta kesi hiyo kwa kiwango ambacho
washtakiwa hao hawatakamatwa tena. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 16,2017
Washitakiwa hao ni mkurugenzi mtendaji,
Benhardard Tito, mwanasheria wa Rahaco, Emmanuel Massawe na mfanyabiashara
ambaye pia ni mwakilishi wa kampuni ya Rothschild (South Africa) Proprietary
Limited, Kanji Mwinyijuma.
Kwa pamoja
wanakabiliwa na mashtaka nane ya uhujumu uchumi likiwamo la matumizi mabaya ya
madaraka, kula njama na kusababisha hasara ya dola za Marekani 527,540.
Washtakiwa hao
wadaiwa kuwa kati ya Septemba Mosi, 2014 na Septemba 30, 2015 kwa nia ya
kutenda kosa walikula njama kinyume cha sheria ya kuzuia na kupambana na
rushwa.
Mkurugenzi Mtendaji
wa kampuni hiyo, Tito, anadaiwa
kuwa Februari 27, 2015 katika ofisi za
Rahaco zilizopo Ilala alitumia madaraka yake vibaya kwa kuiajiri Kampuni ya
Rothschild (South Africa) Proprietary Ltd kama mshauri wa mradi wa uimarishaji
reli ya kati bila idhini ya Bodi ya Zabuni ya Rahaco.
Tito na Massawe
wanadaiwa kuwa Machi 12, 2015 katika ofisi za Rahaco Ilala wakiwa katika
nyadhifa zao, walisaini barua ya kuihalalisha kampuni hiyo ya Afrika Kusini
kuwa mshauri wa mradi wa uimarishaji reli ya kati na kutoa huduma za ushauri wa
kifedha kuhusu mradi huo.
Tito na Massawe
wanadaiwa kuwa Machi 12 na Mei 20, 2015
wilayani Ilala walishindwa kuwasilisha mkataba wa huduma ya ushauri kati ya
kampuni hiyo ya Afrika Kusini na Rahaco.
Tito na Massawe
wanadaiwa Mei 20, 2015 katika ofisi za Rahaco, kwa kutumia madaraka yao vibaya
walisaini mkataba wa kutoa huduma za ushauri na kampuni ya Afrika Kusini bila
ridhaa ya Bodi ya Zabuni ya Rahaco.
Washtakiwa hao,
wanadaiwa kati ya Mei 20 na Juni 20, 2015 walitumia madaraka yao vibaya kwa
kushindwa kuwasilisha mkataba walioingia na kampuni ya Afrika Kusini kwa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Tito, Mwinyijuma na
Massawe, wanaodaiwa kati ya Machi mosi na Septemba 30, 2015 katika ofisi za
Rahaco, waliipa kazi kampuni hiyo ya ushauri na kuilipa kwa kutoa huduma za
ushauri, malipo ambayo yaliisababishia Rahaco kupata hasara ya dola za Marekani
527,540.
Tito anadaiwa Agosti
18, 2015 katika ofisi za Rahaco Ilala, ambapo kwa kutumia madaraka yake vibaya
aliipa Kampuni ya Ujenzi wa Reli ya China kazi ya kujenga kilomita mbili za
reli maeneo ya Soga iliyogharimu dola za Marekani 2,312,229.39 bila idhini ya
Bodi ya Zabuni ya Rahaco.
No comments:
Post a Comment