Hukumu mtoto wa Chacha Wangwe leo...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki
HUKUMU ya kesi ya kuchapisha taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii inayomkabili BOB Chacha Wangwe ambaye ni  mtoto wa mwanasiasa marehemu Chacha Wangwe, itatolewa leo Novemba 15, 2017


Hukumu hiyo inatarajiwa kutolewa na katika Mahakam aya Hakimu Mkazi Kisutu na  Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi siku hiyo  baada ya upande wa Mashtaka kuwaita mashahidi sita kutoka ushahidi kwenye kesi hiyo na mshtakiwa huyo kutoka utetezi wake yeye mwenyewe.

Kwa mujibu wa kesi hiyo  namba 167, 2016 ambayo ilifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Mei 12,2016.

Bob Chacha Wangwe ambaye kitaaluma ni mwana sheria na mwanaharakati wa haki za binadamu anadaiwa kutenda kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa Facebook.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo Machi 15,2016 na kwamba alichapicha maneno haya; “Tanzania ni ambayo….inajaza chuki wananchi … matokeo ya kubaka Demokrasia Zanzibar ni hatari zaidi ya muungano wenyewe…. Haiwezekani nchi ya Zanzibar kuwa koloni la Tanzania bara kwa sababu za kijinga.”



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search