Jakaya Kikwete: Wasanii Tanzania acheni kulialia....soma habari kamli na Matukio360...#share
Na Mwandishi wetu
RAIS mstaafu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Kikwete amewataka wasanii nchini kuacha kulialia na wafanye kazi zenye ubora zitakazowafanya waweza kushindana katika soko la kimataifa
RAIS mstaafu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Kikwete amewataka wasanii nchini kuacha kulialia na wafanye kazi zenye ubora zitakazowafanya waweza kushindana katika soko la kimataifa
Rais mstaaafu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Mrisho
Kikwete akizungumza wakati wa uzinduzi wa Televisheni inayoshughulika na
masuala ya filamu za Kitanzania kwa Wasanii wa Bongo Movie JTV ambayo itapatikana
kupitia king'amuzi cha StarTimes.
Ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye hafla ya uzinduzi wa
Television mpya ya Jason ambayo itakuwa inaonyesha filamu za kitanzania.
“Ni wakati muafaka sasa kwa wasanii kuacha kulia lia kutaka serikali
iwape msadaa, badala yake mfanye kazi zenye ubora zaidi,” amesema na kuongeza
“Msilalamike tu, mkitaka mtoke lazima mfanye kazi nzuri
itakayovuka mipaka ya Tanazania.”
Rais Kikwete amesema ili kufukia hapo ni lazima waweze kuzalisha
filamu nzuri..
Pamoja na hayo Jakaya Kikwete amesema amefurahishwa na muenendo wa tasnia ya sanaa ya filamu, ambayo kwa sasa imetoa ajira kwa watu milioni 6.
Pamoja na hayo Jakaya Kikwete amesema amefurahishwa na muenendo wa tasnia ya sanaa ya filamu, ambayo kwa sasa imetoa ajira kwa watu milioni 6.
Kwa upende mwingine Kampuni ya Star Media (T) Ltd kupitia
chapa yao ya StarTimes walitumia fursa hiyo pia kutangaza kifurushi kipya cha
UHURU kwa wateja wake wa antenna.
Akiongea katika hafla hiyo Meneja Uhusiano wa kampuni
hiyo Juma Suluhu amesema, “Imekuwa ni
shauku yetu siku zote kutoa huduma ya kiwango bora kwa Watanzania na kwa
gharama nafuu kabisa, kifurushi kipya cha UHURU ni ushahidi tosha na tuna hamu
ya kuona wateja wetu pendwa wakikitumia na kufurahia huduma hii.”
“Tumejitolea kuwaletea huduma bora na kiwango cha juu
kabisa, na maono yetu ni kuhakikisha kila familia ya kitanzania inafurahia
huduma za kidigitali na maisha ya kidigitali, hivyo kila tunachofanya ni
kujaribu kutusogeza katika lengo letu hilo na kifurushi kipya cha UHURU ni
hatua kubwa sana.” ameongeza.
No comments:
Post a Comment