Serikali yateketeza makazi kwa milioni 80...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu
SERIKALI wilayani Chunya mkoani Mbeya imetumia milioni 80 katika  operesheni ya  kuwaondoa  na kuteketeza makazi ya wakulima na wafugaji waliovamia  kwenye maeneo ya  hifadhi na misitu ya asili katika tarafa ya  Kipembawe kata ya Kambi katoto.
Baadhi ya nyumba zilizoteketezwa katika zoezi la kuwaondoa wavamizi waliojenga makazi katika maeneo ya hifadhi

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Chunya, Rehema Madusa  alipokuwa  akitoa taarifa ya utekelezaji wa operesheni iliyofanyika kwa siku kumi, kuanzia Oktoba 7, 2017  katika kikao cha kawaida  cha wilaya(DCC) kilichohusisha watendaji wa ngazi za kata, vijiji na wakuu wa idara.

Pia kilijadili sekta ya elimu, kilimo na uwekezaji wa viwanda.

Madusa amesema kaya 18,000 zenye wakazi 9,000 ziliteketezwa na wamelazimika kufanya hivyo kutokana  na uharibifu mkubwa wa mazingira uliofanywa hususan ukataji miti ,uchomaji na kufanya shughuli za kilimo na ufugaji na kusababisha wanyama kukimbia kwenye hifadhi.

"Uharibifu ni mkubwa hasa kwenye maeneo wanayoishi na katikati ya hifadhi. Si rahisi  kutambua uharibifu huo,   hakuna shule, zahanati, maji na nishati ya umeme jambo linalosababisha watoto kukosa haki za msingi ikiwamo ya elimu na  wajawazito kujifungulia katika mazizi ya ng'ombe "amesema.

Madusa amesema kwa sasa wamekwama kuendelea na zoezi hilo kutokana na ukata wa fedha na ameonya watendaji kutotanguliza maslai ya fedha  kwa kuwashawishi kurejea katika maeneo waliyoondolewa  na watakaobainika watawajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Mkurugenzi mtendaji wa wilaya hiyo, Sophia Kumbuli amekea tabia ya watendaji kufumbia macho wavamizi kurejea katika  maeneo waliyoondolewa na watakaobainika  hawatoshi  kuitumikia halmashauri hiyo.

"Nasikia chinichini kuna wakulima na wafugaji walioondolewa wameanza kurejea tena, sasa nashangaa ninyi watendaji mko wapi kwa kweli katika hili siwezi kuvumilia kwani serikali imetumia gharama kubwa na nyinyi wanarejea mnawatazama hapo ni lazima kuna maslai  binafsi," amesema.

Naye Ofisa Maendeleo ya jamii  wilaya, Ally Ally, amesema halmashauri inapata asilimia 65 ya mapato kutoka  katika zao la Tumbaku lakini changamoto ni uharibifu wa mazingira.

Ofisa Mtendaji Tarafa ya Kipembawe, Kassim Kirandomara ameiomba halmashauri kutoa ushirikiano wa haraka  watakapohitaji katika

zoezi la kuwaondoa wavamizi kwa kutuma  askari wa jeshi la polisi

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search