Kabla ya kuivaa Chelsea, Mourihno afikishwa mahakamani...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
KOCHA wa Man United Jose Mourinho amewasili katika mahakama ya Uhispania kujibu madai ya kukwepa kulipa kodi wakati alipokuwa mkufunzi wa klabu ya Real Madrid.

Kocha wa Man united,Jose Mourinho
Wawakilishi wake wamekana kuwa anadaiwa Yuro milioni 3.3 kupitia haki za matangazo ambazo hakuzitangaza.

Mourinho alionekana akiingia mahakamani katika makazi ya mjini Madrid Pozuelo de Alarcon.

Kusikizwa kwa kesi hiyo kunajiri siku moja kabla ya Manchester United kucheza dhidi dhidi ya Chelsea katika ligi ya Uingereza siku ya Jumamosi

Mkufunzi huyo alizungumza na vyombo vya habari siku ya Alhamisi kama ilivyo ada.


Utawala wa Uhispania ulianzisha kesi dhidi ya Mourinho mnamo mwezi Juni.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search