Kikosi wachezaji wapya 'Kilimanjaro Warriors' chatangazwa...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

KOCHA Msaidizi wa timu ya taifa za vijana 'Kilimanjaro Warriors',Oscar Mirambo ametangaza majina ya wachezaji 35 kwa ajili ya kuingia kambini.

Kocha Msaidizi wa timu ya taifa za vijana'Kilimanjaro Warriors' Oscar Mirambo

Lengo la kambi hiyo ni kutafuta kikosi imara cha Taifa kwa vijana wa chini ya umri wa miaka  23 maarufu kwa jina la Kilimanjaro Warriors.

Akitangaza majina hayo Mirambo, amesema “Tunataka vijana wasiozidi 25 kwenye kikosi. Tutawapata kwenye kambi hii ya siku 10 inayoanza Novemba 5, 2017.”

Wachezaji aliowaita ni makipa Metacha Mnata (Azam FC), Joseph Ilunda (JKT Ruvu), Liza Mwafwea (Tanzania Prisons).

Wengine ni Cleotas Sospter (Yanga); Idrissa Mohammed, Bakari Kijuji (Yanga), Joseph Prosper (Azam), Masoud Abdallah (Azam), William (Ruvu Shooting), Yussuph Mhilu (Yanga), Adam Salamba (Stand United), Omary Mponda (Ndanda) na Stanley Angeso (Stand United).

Pia wamo Eliud Ambokire (Mbeya City), Emmanuel Kakuti (Mbeya City), Medson Mwakatunde (Mbeya City), Daruweshi Shaliboko (Ashanti Unted), Abbas Kapombe (Azam/Ndanda), Ismail Aidan (Mtibwa Sugar), Salum Kihimbwa (Mtibwa Sugar), Hassan Mganga (Mtibwa Sugar) na Award Salum (Njombe Mji).

Wengine Awesu Ally (Mwadui), Salum Chuku (Singida United), Yahya Zayd (Azam), Emmanuel Martin (Yanga), Geofrey Mwashiuya (Yanga), Ayoub Masoud (Ndanda), Baraka Majogoro (Ndanda), Mohammed Habib (Miembeni), Yussuf Mlipili (Simba), Agathon Mapunda (Njombe Mji), Faisal Abdallah (JKU) na Yussuph Kagoma (Singida United).


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search