Kesi ya Halima Mdee mhh!!!..soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Abdulrahim Sadiki
KESI ya kutumia lugha ya matusi dhidi ya rais, Dk John Magufuli inayomkabili
mbunge wa jimbo la Kawe(Chadema), Halima Mdee imeshindwa kuanza kusikilizwa kufuatia shahidi kuanza likizo na anasafiri.
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kulia akiwa na mmoja wa mawakili wake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Leo katika Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu, wakili wa serikali, Leonard Challo amemueleza Hakimu Mkazi
Mwandamizi, Victoria Nongwa kesi hiyo
ilipaswa kuanza kusikilizwa leo lakini shahidi waliyemtarajia kuanza kutoka ushahidi ameanza likizo na anasafiri.
Ameomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kuanza
kusikilizwa na siku hiyo wataleta shahidi mwingine.
Hakimu Nongwa ameahirisha
kesi hiyo hadi Desemba 7,2017 kwa ajili
ya kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka. Hatua
hiyo imefikiwa baada ya upelelezi wa kesi hiyo kukamilika.
Katika
usomwaji wa maelezo ya awali ya kesi hiyo (PH), Halima alikumbushwa shtaka
linalomkabili, kuwa alifanya kosa hilo
Julai 3,2017 katika Makao Makuu ya Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema) iliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni.
Kwa kumtukana rais John Magufuli kuwa “anaongea hovyo hovyo , anatakiwa afungwe breki,” kitendo ambacho
kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.
Akisomewa
maelezo ya awali, Halima alikubali maelezo yake binafsi likiwamo jina lake,
anaishi Makongo, yeye ni Mbunge na Siku ya tukio ya Julai 3,2017 alikuwa katika
eneo la ofisi ya Chadema iliyopo mtaa wa Ufipa Kinondoni. Halima
alikana kutoa lugha ya matusi dhidi ya rais Dk John Magufuli.
Akiendelea
kusomewa maelezo hayo ya awali, Halima
alikubali kuwa Julai 4,2017 alikamatwa katika eneo la Kibangu wilaya ya
Kinondoni na kupelekwa katika ofisi ya
ZCO kwa mahojiano.
Hata
hivyo, Halima alikana maelezo ya kuwa wakati akihojiwa alikubali kuwa alitoa
lugha ya matusi dhidi ya rais Magufuli. Pia
Halima alikubali kuwa alifikishwa mahakamani kukabiliana na kesi inayomkabili.
Alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Julai 10,2017.
Katika
kesi hiyo anatetewa na mawakili, Peter Kibatala, Nashon Nkungu, Jeremiah
Mtobesya, Faraja Mangula, Omary Msemo, Hekima Mwasipu.
Tayari
Mdee kupitia mawakili wake amewasilisha pingamizi la awali katika Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi yake
ya kumtolea lugha chafu rais Magufuli.
Wanadai
mapingamizi mawili, kwanza hati ya mashtaka ina mapungufu, pia Mahakama hiyo
haina mamlaka akisema kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka kwa sababu, Mkuu wa
Wilaya aliyetoa amri ya kukamatwa kwa Mdee ameshindwa kufuata matakwa ya
kisheria.
No comments:
Post a Comment