Kinondoni kinara kwa wanaojiuza, bar, migogoro ya ndoa...soma habari kamili na Matukio360..#share

 Na Salha Mohamed
MANISPAA ya Kinondoni jijini Dar es Salaam ina Bar nyingi zaidi kuliko wilaya nyingine nchini,  ina migogoro 1134 ya ndoa na watu wanaojiuza kimapenzi.


Mwenyekiti wa kamati maalum ya kurekebisha sheria za usalama barabarani, Deus Sokoni akizungumza na waandishi wa habari
Hayo yamesemwa na Ofisa Ustawi wa Jamii Manispaa hiyo, Judith Kimaro katika mkutano wa ukusanyaji maoni kutoka kwa wadau kupata sera ya udhibiti wa pombe nchini yaliyoandaliwa na Chama cha Afya ya Jamii.

Amesema manispaa hiyo imesajili Bar 2069 na  mwaka 2016/17 imesuluhisha migogoro 76  ya watu kuacha matumizi ya pombe kupindukia iliyowasilishwa katika manispaa hiyo.

“Madhara ya pombe ni makubwa, tumeweza kusuluhisha migogoro 266 iliyosababishwa na pombe iliyopindukia na watoto wengi wamebaki yatima kutokana na vifo vya wazazi wao,”amesma.

Kimaro amesema mwaka 2016/2017 kumekuwa na kesi zipatazo 40 ambazo zipo mahakamani zinazotokana na ubakaji na ukatili wa kijinsia kutokana na matumizi ya pombe.

Amesema katika manispaa hiyo kuna migogoro 7 65 ya familia ambayo inaendelea kusuluhishwa na familia 27 zimesambaratika mwaka 2016/2017.

“Kutokana na hali hiyo, Kinondoni kumekuwa na ongezeko la watu wanaojiuza kwa jinsia zote kama Sinza, Magomeni Kagera lakini huwa tunawatembelea na kuwashauri,”amesema.

Ameitaka serikali kutoa elimu ya madhara ya pombe, kuweka mitaala ya madhara ya pombe kwa ngazi ya elimu ya msingi na serikali hadi vyuo na kuweka kipaumbele katika mapambano dhidi ya pombe kama ambavyo imeweka katika maambukizi ya Malaria na virusi vya Ukimwi.

Mwenyekiti wa kamati maalum ya kurekebisha sheria za usalama barabarani, Deus Sokoni amesema kuna haja ya kurekebisha sheria ya matumizi ya pombe ili iendane na viwango vya kimataifa.

‘Kuna haja ya kuboresha sheria lakini tumeweka adhabu kali kwa dereva atakayesababisha ajali tumependekeza adhabu kali kwa dereva atakayeendesha gari akiwa amelewa adhabu iwe kuanzia sh 500,000 na kuendela,”amesema.

Amesema Januari hadi Septemba, 2017 takribani madereva 22804 walikamatwa wakiendesha gari wakiwa wamelewa na madereva 71 walisababisha ajali na vifo vya zaidi ya watu 300 kufariki.

Amesema lengo  hadi kufikia mwaka 2020 ni kupunguza ajali kwa asilimia 50 na kuwa hawambembelezi dereva mlevi.
 Mratibu wa Mradi wa kupunguza matumizi ya pombe, Irene Charamila amesema mradi huo  ni wa awamu ya pili umeanza 2017 hadi 2021.

“Tulifanya utafiti kwa Wilaya za Mkuranga, Mbulu na Monduli lakini Wilaya ya Mbulu katika Kata ya Sanubaray na Dongobesh ilionekana kuwa na matumizi makubwa ya pombe,”amesema.

Amesema katika wilaya hiyo wanawake wanakilio cha waume zao kutumia pombe kupita kiasi na kutohudumia familia na wanahitaji haraka sera ya udhibiti wa pombe.

Mmoja wa wanachama hao, Daktari Geofrey Swai amesema matumizi ya pombe huaribu akili ya mtu na kumfanya kupooza na hata kupoteza fahamu na hubadilika tabia  na kutetemeka mwili  anapoikosa.
“Mtu akinywa pombe husababisha ini kukauka na kuwa na kambakamba na hatimaye kushindwa kufanya kazi, kupata saratani ya kongosho, saratani ya mdomo, satarani ya koromeo, kusababisha ugomvi na hata kunywa sumu,”amesema.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search