DPP 'amuokoa' Adam Malima...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi wetu
MKURUGENZI wa Mashtaka(DPP) ameondoa nia ya kuendelea na kesi ya shambulio iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa naibu waziri wa fedha katika serikali ya awamu ya nne, Adam Kighoma Malima na Ramadhani Mohammed Kigwande

Adama Malima kushoto akitoka Mahakamani.
Kufuatia hatua hiyo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeifuta rasmi kesi  hiyo na Hakimu mkazi mkuu, Respicius Mwijage kuwaachia huru washtakiwa hao baada ya wakili wa serikali mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kuomba ifutwe chini ya kifungu cha 91 (1) cha mwenendo wa Mashauri ya Jinai kwa sababu Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) hana nia ya kuendeleza mashtaka hayo dhidi yao.

Kishenyi amesoma kifungu hicho ambacho kinampa mamlaka DPP kuiondoa kesi mahakamani  wakati wowote pale anapoona inafaa na pia kinamruhusu kuirudisha mahakamani pia.

Baada ya Kishenyi kukisoma kifungu hicho, Hakimu Mwijage alikubali na kuwaachia huru washtakiwa wote.

Kesi hiyo ilikuwa katika hatua ya usikilizwaji wa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Awali, wakisomewa melezo ya awali (PH),  Malima na mwenzake Ramadhani Mohammed walikubali maelezo  binafsi, siku ya tukio walikuwepo Masaki, walikamatwa na kushtakiwa na wakayakana mashtaka yote yanayowakabili.

Katika kesi hiyo, Malima anadaiwa kuwa Mei 15,2017 katika eneo la Masaki kwa makusudi alimzuia ofisa wa polisi H.7818 PC ABDU kufanya kazi yake halali.


Malima anadaiwa   kumzuia afisa huyo kufanya kazi yake ya kumkamata Ramadhani Kigwande kwa kosa la kumshambulia Mwita Joseph.

Kwa upande wa mshtakiwa wa kwanza, Ramadhani Mohammed Kigwande Naye anakabiliwa na shtaka la kumshambulia Mwita Joseph.

Ilidaiwa kuwa siku hiyo ya Mei 15,2017 kwenye eneo hilo la Masaki wilaya ya Kinondoni mshtakiwa Ramadhani  akiwa na nia ya kumzuia Mwita Joseph ambaye ni afisa oparesheni wa kampuni ya Priscane Business Enterprises  wakati alipokuwa akimkamata kwa kupaki vibaya gari namba T 587 DDL alimshambulia na kumsababishia maumivu.


Baada ya kusomewa mashtaka hayo,washtakiwa wote walikana na  walikuwa nje kwa dhamana kwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja ambaye alisaini bondi ya milioni  5.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search