Kotei:Sikuja Tanzania kutalii..Soma habari kamili na Matukio360...#share


 Na mwandishi wetu

KIUNGO Mghana wa Simba, James kotei amesema hakuja Tanzania kutalii bali kufanya kazi ndiyo maana amekuwa akijituma ili kuisaidia timu hiyo kufanya vizuri.

James Kotei

Akizungumza baada ya mchezo kati ya Simba na Mbeya City jana, Kotei alisema kamwe hatabweteka badala yake ataendelea kupambana ili awe bora zaidi na kutoa mchango unaohitajika kwa waajiri wake.

"Mpira ndio kazi yangu, sikuja hapa kukaa benchi, nimekuja kucheza ndio maana namudu kucheza nafasi nyingi uwanjani.

“Nimejipanga kuisaidia Simba kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa mwakani,pia itakuwa fursa kwangu ya kujitangaza.

"Bado nina safari ndefu katika soka,lengo langu sio kuishia kucheza Tanzania,nataka kusonga mbele,”alisema Kotei.

Kotei anayemudu kucheza nafasi zote za ulinzi na kiungo jana alikuwa na mchango mkubwa katika kikosi cha Simba kilichoibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City,Uwanja wa Sokoine,Mbeya.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search