Kocha : ‘Kilimanjaro Queens’ inakibarua kizito kutetea taji...Soma habari kamili na Matukio360..#share


 NA MWANDISHI WETU

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya wanawake ‘Kilimanjaro Queens’ inayotarajia kushiriki mashindano Kombe la Chalenji( Cecafa Cup)nchini Rwanda,  Sebastian Nkoma amesema Tanzania  inakibarua kizito kutetea taji lao mwaka huu.

Timu ya Kilimanjaro Queens

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Nkoma amesema ili kutetea ubingwa wa michuano hiyo wanaoushikiria wanahitaji kufanya maandalizi ya uhakika,lakini kinyume na hapo itawawia vigumu.

Nkoma amesema hadi sasa hajapewa muelekeo wa kambi ya timu hiyo licha ya kuwasilisha  program yake tangu  Oktoba mwaka huu.

“Washiriki wengine watakaokuja kwenye mashindano hayo wamelenga kuchukua taji ambalo sisi tunalitetea, ndio maana ninasema kutetea taji ni shuguli ngumu kuliko kuliwania kama wenzetu watakavyokuwa wakifanya.

“Ninachofahamu mashindano haya yaliyokuwa yamepangwa kufanyika Novemba, yamesogezwa mbele hadi Desemba ingawa tarehe rasmi haijajulikana,”amesema Nkoma.

Nkoma amesema maandalizi ya mapema yanawasaidia wachezaji kujipanga badala ya kukurupushwa kitu ambacho kitawafanya washindwe kufanya vizuri.


Tanzania ilifanikiwa ubingwa ubingwa wa  michuano hiyo  mwaka 2016 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1  dhidi ya Kenya katika mchezo wa fainali.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search