Mahakama yapiga marufuku 'vishoka'...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MAHAKAMA imepinga vikali vitendo vya ulaghai  ikiwamo vya mawakili feki na vishoka vinavyofanywa na baadhi ya wananchi kwa lengo la kujipatia kipato.


Ni baada ya tukio la  Jeremiah Ragita aliyejifanya kuwa Wakili akitokea Kampuni ya Sheria ya Faithful Attorney Advocates.

Naibu Msajili,  Mahakama ya Ardhi, Frank Mahimbali anasema Wakili huyo feki alikamatwa mapema Novemba 8, 2017  katika Mahakama hiyo akimsimamia Mleta maombi Nunu Mhusin Mkwata.

Mahimbali amesema kuwa upande wa pili ambao unasimamiwa na Wakili Maros Gabriel kutoka Kampuni ya Sheria ya 'Common Law Chambers' ulimtilia shakaJeremiah Ragita kama kweli ni Wakili ndipo alipofanya upekuzi kwenye Ofisi ya TLS na kuambiwa kuwa hawana jina hilo.

Hata hivyo, Mahimbali anasema Maros alienda  mbali kwa  kumuandikia barua Msajili wa Mahakama Kuu (RHC) na kujibiwa kuwa hakuna Wakili aliyesajiliwa kwa jina hilo.

Kwa mujibu wa Naibu Msajili kesi hiyo ilipoitwa mbele ya  Jaji Crencesia Makuru, Wakili Maros alimueleza  Jaji huyo kuwa mwenzake wa upande wa pili sio Wakili na kisha akatoa vielelezo kutoka katika Ofisi ya Msajili Mahakama Kuu na Ofisi ya TLS ndipo Ragita akakiri kuwa yeye si Wakili.

Hata hivyo, Ragita alikamatwa na kupelekwa Polisi Kituo cha Kati (Central Police) jijini Dar es Salaam kwa ajili ya hatua stahiki za kisheria.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search