Vigogo walia njaa mahakamani...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na Abdulrahim Sadiki
MKURUGENZI
wa Tathmini, Archard Alphonce Kalugendo (49) na Mthamini wa Madini ya Almas wa
Serikali, Edward Joseph Rweyemamu (50) wamezidi kuiomba Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu isaidie familia zao kupata
mishahara yao.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Washtakiwa
hao, kupitia wakili, Nehemia Nkoko walitoa ombi hilo leo mbele ya Hakimu Mkazi
Mkuu, Respicius Mwijage wakati kesi hiyo ilipotajwa.
Nkoko
ameomba mahakama isaidie familia za washtakiwa hao kupata mishahara hiyo kwa
sababu wana watoto ambao wanahitaji huduma na wanaugua.
"Tungependa
washtakiwa wapate dhamana lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amewawekea zuio
la dhamana hivyo tunaomba wapatiwe mishahara yao hata kwa kupitia dirishani
halafu wao waendelee kushikilia hizo akaunti," ameeleza Nehemia.
Nehemia
ameyaeleza hayo leo mara baada ya Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kudai jalada
la polisi la kesi hiyo lipo kwa DPP na kwamba tarehe ijayo wataeleza kwa
ufasaha upelelezi wa kesi hiyo umefikia
wapi.
Kwa
upande wa Wakili mwingine wa utetezi, Ludovick yeye alidai kuwa washtakiwa hao
walishikiliwa polisi kwa takribani wiki tatu wakisema wanachunguza
wakikamilisha watawapeleka mahakamani, tumaini la upande wa utetezi ni
walipoletwa mahakamani upelelezi umekamilika.
Hivyo
aliomba upande wa Mashtaka kueleza ni sehemu gani ambayo upelelezi bado kwa
sababu wao wanaamini hadi washtakiwa hao wanaletwa mahakamani upelelezi
umekamilika.
Baada
ya kutolewa kwa hoja hizo, Wakili wa Serikali, Wankyo alimshauri wakili Nkoko
kuandika barua kwa DPP ili aweze kushughulikia suala hilo.
Nehemia
alisisitiza kuomba familia za washtakiwa hao zipatiwe mishahara hiyo kwa sababu
chanzo chake kinajulikana kinatoka wapi na kwamba familia hizo zinahaki ya
kupata mahitaji na kuzuia ni kuwahukumu.
Hakimu
Mwijage aliamuru upande wa Mashtaka na utetezi kushirikiana kulishughulikia
familia hizo zipate mishahara hiyo na
Novemba ,23,2017 wapeleke taarifa.
Pia
aliamuru upande wa Mashtaka siku hiyo kupeleka mahakamani hapo taarifa
inayoeleweka kuhusiana na upelelezi umefikia wapi.
Washtakiwa
hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa
kusababisha hasara ya dola za Kimarekani 1,118,291.43 sawa na Sh
2,486,397,982.54.
Kalugendo
ambaye ni Mkazi wa Kinyerezi na Rweyemamu Mkazi wa Mwananyamala wote ni
waajiriwa wa Wizara ya Nishati na
Madini.
Kati
ya Agosti 25 na ,31, 2017 katika maeneo mbalimbali kati ya Dar es Salaam na
Shinyanga, washtakiwa hao kwa pamoja na kwa vitendo vyao wakiwa wathamini
walioajiliwa na Wizara ya Nishati na Madini walisababisha hasara ya kiasi hicho
cha fedha.
Baada
ya kusomewa shtaka hilo, washtakiwa hao hawakuruhusiwa kuongea chochote kwa
sababu Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hadi Mahakama
Kuu Kitengo cha Rushwa na Uhujumu Uchumi maarufu Mahakama ya Mafisadi. Washtakiwa
wapo rumande.
No comments:
Post a Comment