Makamu wa rais aongoza matembezi ya hisani kuchangisha fedha kusomesha wauguzi, wakunga...Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan, leo ameongoza matembezi ya hisania ya kilometa nne na nusu yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga.

Makamu wa Rais Samia Ssuluhu Hassan akizungumza jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, huku wakitembea wakati wa matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha Wauguzi Wakunga jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Samia Ssuluhu Hassan akizungumza jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, huku wakitembea wakati wa matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha Wauguzi Wakunga jijini Dar es Salaam.
Akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Green Ground- Oysterbay mara baada ya matembezi hayo, Makamu wa Rais alisema takwimu za vifo vya kina mama zimeongezeka, hivyo wazo la kusaida kuongeza idadi ya wakunga ambao watasaidia kupunguza vifo hivyo ni zuri.
Amesema “nimefarijika kusikia kuwa mwaka 2016 matembezi haya ya hisani yalikusanya wastani wa sh. milioni 290 pesa ambayo iliwekwa katika fungu la kusomesha wauguzi wakunga wapya 75 katika mafunzo ya ngazi ya cheti,” amesema.
Amesema “nimefarijika kusikia kuwa mwaka 2016 matembezi haya ya hisani yalikusanya wastani wa sh. milioni 290 pesa ambayo iliwekwa katika fungu la kusomesha wauguzi wakunga wapya 75 katika mafunzo ya ngazi ya cheti,” amesema.
Aidha ameonesha kufurahishwa na malengo yaliyowekwa kwa miaka miwili ijayo ya kukusanya kiasi cha sh. milioni 300 kwa ajili ya kusomesha wakunga wauguzi 400 katika ngazi ya cheti na diploma kwa njia ya masafa.
Makamu wa Rais amesisitiza kuwa moja ya chanzo cha vifo vya kina mama na watoto wakati wa kujifungua ni ukosefu wa wataalam wa kuwahudumia. Takwimu za Tanzania zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya akina mama hawaendi kujifungua katika vituo vyetu vya kutolea huduma kutokana na kukosekana kwa wataalam wa kuwahudumia akina mama hao.
Matembezi yakiendelea
Picha ya pamoja na Washiriki wa Matembezi hayo ya Hisani.
No comments:
Post a Comment