JUKATA kumfungulia kesi mwanasheria mkuu wa serikali..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed
JUKWAA la Katiba Tanzania (JUKATA), linatarajia kumfungulia  kesi  Mwanasheri Mkuu wa Serikali (AG) likidai kuminywa na kuzuiwa na Jeshi la Polisi kufanya maandamano ya amani Oktoba 30, 2017.



Mwenyekiti wa Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA), Hebron Mwakagenda (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo na kutoa maamuzi ya Jukwaa baada y kukataliwa kufanya Maandamano ya amani Oktoba 30, 2017. Kushoto ni Msafiri Shabani Mjumbe na Marganius Msambila ambaye pia na mjumbe. 
Maandamano hayo yalilenga kuunga mkono jitihadi za rais John Magufuli katika kusimamia rasilimali za taifa pamoja na kupiga vita rushwa.

Mwenyekiti wa Jukwaa hilo,  Hebron Mwakagenda  leo jijini Dar es salaam amesema hawajapokea barua ya kukubaliwa kufanya maandamano hayo kutoka Ikulu na walipokea barua kutoka jeshi la Polisi kanda  Maalum likiwakataza kufanya maandamano.

"Tumefanya uchambuzi wa sababu zilizotolewa na kuridhika kwamba ipo haja ya kuchukua hatua zaidi.... Jeshi la Polisi liliainisha sababu tatu, "amesema.

Amesema sababu hizo ni rais kutothibitisha kushiriki kwenye maandamano, kufanya maandamano ya umbali mrefu kwa kufunga barabara  kutaathiri shughuli na Oktoba 30,2017 wanafunzi wa kidato cha nne wanafanya mitihani.

"Kwasababu hizi zilizotumika JUKATA tumefikia maamuzi ya kwenda kufungua kesi mahakamani kudai haki ambayo inaminywa na kukandamizwa na Jeshi la Polisi kwa kutumia sababu nyepesi, "amesema.

Amesema wapo kwenye hatua za mwisho  kutekeleza uamuzi huo na kwamba jopo la mawakili wasiopungua kumi wakiongozwa na Dk. Rugemeleza Nshala watahusika katika mchakato huo.

Mwakagenda amesema miongoni ma sababu zinazosababisha kwenda mahakamani ni kuomba tafsiri ya mahakama kuhusu namna jeshi la Polisi linavyotumia kifungu 43(3) na 44 ya sheria ya Jeshi la Polisi ya mwaka 2002.

"Kwa mtazamo wa uchambuzi wetu Jeshi la Polisi limekuwa likitumia vibaya vifungu hivi kuzuia mikutano pamoja na maandamano ya amani kinyume na uhalisia wa vifungu hivi kwa kisingizio cha uwepo wa taarifa za kiintelijensia kuwa kuna viashiria vya uvunjifu wa amani,  "amesema.

Akizungumzia suala la katiba mpya,  Mwakagenda amesema jukwaa hilo linaendelea kusisitiza haja na umuhimu wa kukamilishwa kwa mchakato huo.

Amesema imethibitika kuwa asilimia 67 ya wananchi wanaona ni muhimu Tanzania kupata katiba mpya.

" Ni muhimu serikali kutekeleza jambo hili kwakuwa pia lipo kwenye ilani ya uchaguzi ya chama tawala, CCM. "...tunasisitiza serikali kufanya marekebisho kwenye katiba ya sasa endapo mchakato wa katika haujakamilika 2020  wakati a uchaguzi ili kuondoa dosari ambazo zimekuwa zikilalamikiwa kila uchaguzi, "amesema.
           


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search