Mboga mboga, matunda chanzo cha maradhi...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na
Salha Mohamed
UTAFITI unaeleza kuwa viashiria vya magonjwa yasiyoambukiza unaongezeka kutokana na ulaji wa mboga mboga na matunda kuwa chini ya kiwango.
Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Neema Rugemayila, akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya kisukari duniani na kampeni ya mazoezi jijini Dar es Salaam.
Utafiti huo umefanywa na Wizara y Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) mwaka 2012.
Hayo yamebanishwa Dar es Salaam leo na Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Neema Rugemayila wakati wa maadhimisho ya siku ya kisukari
duniani na kampeni ya mazoezi.
Amesema silimia 97.2 ya wananchi wanakula mboga mboga na matunda chini ya mara tano kwa wiki nchini.
Utafiti huo unaonesha kuna ongezeko kubwa la viashiria
hivyo linalochangiwa na uvutaji wa sigara na kuwa asilimia 15.9 ya wananchi wanavuta sigara.
"Asilimia 29.3 wanakunywa pombe, asilimia
97.2 wanakula mboga mboga na matunda chini ya mara tano kwa wiki,
"amesema.
Amesema asilimia 26 ya wananchi ni wanene kupita kiasi, asilimia
26 wanalehemu nyingi mwilini, asilimia 33.8 wanamafuta mafuta mengi mwilini
huku asilimia 9 waligundulika kuwa na kisukari.
Amesema utafiti huo pia ulionesha asilimia 25 ya wananchi
waliohojiwa hawajishughulishi na kazi zinazotumia nguvu na kutofanya
mazoezi.
"Viashiria ambayo tunapaswa kupambana navyo ili tupambane na
magonjwa yasiyoambukiza ni unywaji pombe kupita kiasi, matumizi ya tumbaku na
bidhaa zake, ulaji usiofaa hasa matumizi ya chumvi kwa wingi,
mafuta,sukari sukari na kutofanya mazoezi.
Amesema asilimia 6 ya vifo duniani husababisha na kutofanya
mazoezi ambapo imetajwa kuwa ni kiashiria cha nne kinachochangia vifo
duniani.
"Inadaiwa kuwa kutofanya mazoezi kunachagia asilimia
17 ya magonjwa ya moyo na kisukari, asilimia 12 ya matatizo ya kuanguka
na asilimia 10 ya saratani ya utumbo maana, "amesema.
Amesema kwa mujibu wa Shirika la afya duniani(2005), inakadiriwa
kuwa asilimia 20 ya vifo vyote vilivyotokea hapa nchini vinatokana na magonjwa
yasiyoambukiza.
Kwa upande wake rais wa Club ya Lion kwa nchi za Tanzania,
Uganda na Sudani kusini, Rowan Qadri amesema wanatoa huduma kwa wagonjwa a
kisukari bure kwa wiki moja.
Amesema kwa pamoja wanaweza kushinda ugonjwa huo hivyo wafunge
miili yao ili kupambana a ugonjwa huo.
Naye Mkurugenzi wa Kinga dhidi ya magonjwa sugu Dk Manase Frank
amesema watu wengi wanafariki au kuumia kutokana kutokana na ugonjwa wa
kisukari.
Amewataka viongozi wa dini kuwahubiria waumini kupima afya zao
angalau mara moja kwa mwaka.
No comments:
Post a Comment