Mbunge ataka wabunge walipwe pensheni...Soma habari kamili na Matukio360...#share


Na mwandishiwetu

SERIKALI imeombwa kuanza kuwalipa pensheni wabunge baada ya kuachia wadhifa huo.

Bungeni

Ombi hilo limetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia katika kipindi cha maswali na majibu.

Katika swali lake la kwanza Mbatia aliuliza utaratibu wa kuwahudumia Majaji wastaafu hususani wanapoumwa.

Mbatia amesema sheria ya mwaka 1981  ilielekeza kulipa pensheni wabunge waliondoka katika wadhifa huo na kwamba sasa ni wakati muafaka kwaserikali kuangalia upya utoaji wapensheni kwa wabunge.

“Sheria ya mwaka 1981 kabla yakufutwa ilielekeza wabunge kulipwa pensheni sasa ni muda muafaka kwa serikali kuwapa pensheni wabunge,” aliuliza Mbatia.

Akijibu hoja hiyo Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Antony Mavunde amesema kwakuwa swali ni ombi serikali kabla haijatoa kauli rasmi itaangalia taratibu,  sera na sheria ya pensheni ya mwaka 2007  inavyoelekeza.

“Kabla serikali haijatoa tamko rasmi kuhusu ombi hilo,  itaangalia taratibu, sera na sheria ya pesheni ya mwaka 2007 inavyoelekeza katika suala hilo,” alijibu Mavunde

Kuhusu Majaji Wastaafu, serikali imesema wanahudumiwa kwamujibu wa sheria na taratibu zinavyoelekeza.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search