Tanzania yaijibu Kenya…Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

SERIKALI ya Tanzania imeitaka Serikali ya Kenya kusubiri majibu sahihi kuhusu ukamatwaji wa vifaranga na mifugo iliyoingizwa nchini hivi karibuni bila kufuata taratibu na sheria.  
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Augustine Mahiga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Augustine Mahiga alipozungumza na waandishi wa habari.

Hatua hiyo inafuatia uchomwaji wa vifaranga vya kuku wa mayai takribani 6,400 katika eneo la Namanga Mpakani mwa Tanzania na Kenya ikidaiwa kuingizwa kimagendo. Pia ng’ombe zaidi ya 1,000 walioingizwa kinyemela kwa ajili ya malisho.

“Tanzania inatayarisha maelezo, hata bungeni  kulikuwa na maswali na tumeandaa majibu kufafanua tatizo hili,” amesema Dk. Mahiga.

Amesema kwa njisi tatizo hilo linavyoripotiwa linaleta sintofahamu kwa nchi zote mbili.

Dk. Mahiga amesema zipo  sheria na taratibu za mifugo ambazo hazimo kwenye makubaliano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Amesema  majibu ya suala hilo yatatolewa na wizara yake na wizara ya  mifugo na uvuvi.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search