MOI kujenga maabara ya kisasa...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed
TAASISI ya Tiba ya Mifupa(MOI),  imesema maabara ya kisasa itakayopima vipimo vyote vya damu itaanzishwa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa jengo la MOI awamu ya tatu. 

Meneja Uhusiano Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI)  Jumaa  Almasi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  mafanikio ya taasisi hiyo na kumpongeza rais John Magufuli katika kipindi cha miaka miwili leo Jijini Dar es Salaam, kushoto ni ofisa Uhusiano wa taasisi hiyo Patrick Mvungi.

Pia imesema serikali imetoa bilioni 16.5 kununua vifaa tiba vya uchunguzi ikiwamo CT-Scan, MRI,  X-ray 2, C-arm  na ultrasound ya kisasa.

Hayo yamesemwa Dar es Salaam  na Meneja uhusiano wa Taasisi hiyo, Jumaa Almas wakati akizungumza na waandishi wa habari alipokuwa akizungumzia mafanikio yaliyopatikna katika kipindi cha miaka miwili( 2015/2017)  na jitihada za rais Magufuli katika sekta ya afya.

Amesema kukamilika kwa jengo hilo kutaanzishwa kwa maabara ya kisasa ambayo itafanya vipimo vyote vya damu, kuongeza vitanda vya ICU kutoka vitanda 8 hadi 32.

"Kutaanzishwa kwa kitengo kipya cha kisasa cha wagonjwa ya dharura na tutaongeza  vyumba viwili vya upasuaji na kufanya taasisi kuwa na vitanda 8,"amesema.

Amesema katika kipindi cha miaka miwili taasisi hiyo  imetengeneza viungo bandia 1362  kutokana na serikali kurahisisha upatikanaji w malighafi za kutengeneza hapa nchini ambapo awali wengi walihitaji kupelekwa nje ya nchi kwa gharama kubwa.

Amesema wamekuwa na ongezeko la wagonjwa wanaopewa huduma za kibingwa (Super Specialised services) ambapo wamefanya upasuaji mkubwa kwa wagonjwa 221 wa nyonga(Total hip replacement.

Almas ameongeza wamefanya upasuaji wa mgongo kwa wagonjwa 259(Specialized spine survey),  306 wagonjwa wa ubongo(Specialized brain surgery), upasuaji wa matundu (Athroscopy)  kwa wagonjwa 314, watoto wenye vichwa vikubwa a mgongo wazi (Hydrocephalus and Spina bifida)  852, wagonjwa 120 wa upasuaji wa magoti (Total Knee replacement), Upasuaji wa mfupa wa kiuno (Acetabular reconstruction)  kwa wagonjwa 114.

"Upasuaji mwingine wa mifupa tumefanya kwa wagonjwa 8615.Idadi ya wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji imeongeza kutoka wagonjwa 300-400kwa mwezi  hadi kufikia wagonjwa 600-700 kwa mwezi,"amesema.

Almas amesema "Hili limewezekana kutokana na serikali kuongeza upatikanaji wa vifaa tiba na nafasi ya kulaza wagonjwa ambapo awali ilikuwa finyu," amesema.

Amesema awali mazingira ya kutokea huduma yalikuwa hatarishi kwa watumishi na wagonjwa kupata maambukizi kutokana na ufinyu wa nafasi na idadi kubwa ya wagonjwa.

Amesema kuanza kukamilika kwa mradi wa awamu ya tatu kumesababisha mazingira ya kazi kuwa rafiki kwa watoa huduma n wagonjwa pia.

"Idadi ya wagonjwa ilikuwa kubwa kwa mfano wodi ya yenye vitanda 33 ilikuwa inalaza wagonjwa 90 hadi 100,"amesema Almas.

Amesema katika kipindi cha miaka miwili taasisi hiyo imeongeza idadi ya vitanda kutoka 159 hadi kufikia vitanda 340 baada a rais Magufuli kutoa maelekezo ya wagonjwa kutopata huduma wakiwa wamelazwa chini.


"Kimsingi suala la wagonjwa kulala chini MOI limebaki historia, mazingira ya kutoa huduma yameboreshwa, "amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search