Maalbino kutibiwa bure...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
SERIKALI ipo katika mkakati wa kuandaa  utaratibu na sera ya matibabu bure kwa watu wenye ulemavu wa ngozi(Albino)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijibu maswali Bungeni

Pia itawadhibiti wafanyabiashara wanaouza mafuta ya ngozi ya Albino kwa bei ya juu.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na naibu waziri ofisi ya waziri mkuu, Stella Alex Ikupa alipokuwa akijibu swali la mbunge juu ya mpango wa serikali kuondoa kodi ya dawa na mafuta ya ngozi yanayotumiwa na Albino.

"Pamoja na mambo mengine Serikali inaanda utaratibu na sera ya matibabu bure kwa watu wenye ulemavu wa ngozi(Albino). Pia itawadhibiti wote wanaouza dawa na mafuta ya ngozi ya Albino kwa bei ya juu," amesema Ikupa

Amesema serikali imeshaondoa kodi ya dawa zote za watu wenye ulemavu ikiwamo mafuta ya ngozi ya albino.


Kuhusu upungufu wa dawa naibu waziri huyo amesema serikali itaendelea kuagiza dawa za Albino kadri itakavyohitajika.
"Serikali itaendelea kuagiza dawa za watu  wenye ulemavu wa ngozi kadri zitakavyohitajika," amesema

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search