Msemaji wa Serikali: Nchi imetikisika!...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MSEMAJI mkuu wa serikali na mkurugenzi mkuu wa idara ya habari maelezo, Dk Hassan Abass amesema  kwa sasa nchi imepata mshtuko.

Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari Maelezo, Dk Hassan Abass

Amesema hayo leo jijini Dar es salaam alipokuwa akitoa tathmini ya miaka miwili ya serikali ya awamu ya tano tangu iingie madarakani Novemba 5, 2015.

 “Pamoja na mambo mengine changamoto katika miaka hii miwili ya uongozi wa rais Dk Magufuli  ni mshtuko wa ndani na nje ya nchi ya jinsi Tanzania inavyofanya shughuli zake, nchi imetikisika,” amesema Abbas

Amesema imetigisika kufuatia wapiga dili  kushindwa kufanikisha mipango yao ya kujipatia kipato kwa njia ya ‘ujanja’ kutokana na mianya yote kubanwa na kudhibitiwa ipasavyo na serikali.

Dk Abass amesema kutokana na hali hiyo wapo watu wa ndani na nje ya nchi wasiofurahia jitihada hizo na amewataka  watanzania kushikamana katika hilo na  kudhibiti maslahi ya taifa.

“Wengi wa wapiga dili ambao walizoea kujipatia fedha ndivyo sivyo wameshikwaa na butwaa na hawafurahia hali hii, ukweli mianya imebanwa ipasavyo hivyo si wa ndani wala wa nje hawafurahii hali hii,” amesema Abass.

Kuhusu mafanikio katika sekta mbalimbali amesema  serikali imefanya jitihada za kutosha na kwamba mafanikio yanaanza kuonekana.

 Katika sekta ya elimu amesema kila mwezi serikali inatoa bilioni 23  kugharamia elimu bure, sekta ya afya  dawa zinapatikana na uanzishwaji wa viwanda vitakavyosaidia kupunguza tatizo la ajira nchini.

Msemaji huyo wa serikali amesema hadi kufikia mwisho wa Novemba, 2017 serikali itapandisha madaraja wafanyakazi na kuongeza  mishahara.

“Pia serikali inatoa ajira 52000 katika sekta mbalimbali hii ni kabla ya mwisho wa bajeti tayari zingine zimeanza kutangazwa ikiwamo maafisa kodi wa TRA, maafisa wa afya. Na imewafukuza watumishi takribni 1200 wa vyeti feki na elfu ishirini hewa,” amesema

 Kuhusu ndege, amesema hadi kufikia Julai, 2018 ndege zote zilizonunuliwa na serikali zitafika nchini.


“Ndege ya Boing itaingi Julai na  cc series zitaingia June, 2017 nyingine zipo katika majaribio na hadi mwakani  mwanzoni zitakuwa zimefika nchini,” amesema

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search