ACT wampa neno rais Magufuli...soma habari kamili na matukio360..#share

Abraham Ntambara
CHAMA cha ACT-Wazalendo kimemtaka rais Dk John Magufuli kuacha
kuongoza nchi kibaguzi ili akumbukwe kwa historia njema atakapomaliza uongozi wake
Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Yeremia Maganja (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ( pichami hawapo)
Pia kimesema mwenyekiti na katibu mkuu wa chama hicho wataitikia wito wa Jeshi la Polisi kwenda kuripoti kwa Mkurugenzi wa
Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kitengo cha Makosa ya Fedha (Financial
Crime) na si kamati kuu ya chama hicho.
Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es salaam na kaimu mwenyekiti wa chama hicho, Yeremia Maganja alipozungumza na waandishi wa habari na kwamba rais Magufuli na CCM wanasera ya kubagua watu kwa misingi ya kisiasa.
Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es salaam na kaimu mwenyekiti wa chama hicho, Yeremia Maganja alipozungumza na waandishi wa habari na kwamba rais Magufuli na CCM wanasera ya kubagua watu kwa misingi ya kisiasa.
“Magufuli amesahau kwamba alipata asilimia 58 za kura,
upinzani ulipata asilimia 42, kwa hiyo katika kila watanzania 10 kuna
watanzania 4 wa vyama mbadala, hawa ni Watanzania ambao kijamii wanabaguliwa,”
amesema Maganja.
Amesema kwa sasa watu wanaotoa maoni au
mawazo mbadala na serikali wanachukiwa na kukumbwa na misukosuko ikiwemo kukamatwa
na jeshi la polisi.
Maganja amesema taifa lisilohoji ni taifa la wajinga na ametaka kuwapo kwa uhuru wa maoni kwa kila mtanzania.
Kuhusu wito wa kuitwa na jeshi la polis, Maganja amesema Novemba 2, 2017 walipokea wito huo ukiwataka wajumbe wa kamati kuu ya ACT-Wazalendo kufika kituo cha pilisi cha Kamata, Kariakoo jijini Dar es Salaam kwenda kuhojiwa na DCI.
Kuhusu wito wa kuitwa na jeshi la polis, Maganja amesema Novemba 2, 2017 walipokea wito huo ukiwataka wajumbe wa kamati kuu ya ACT-Wazalendo kufika kituo cha pilisi cha Kamata, Kariakoo jijini Dar es Salaam kwenda kuhojiwa na DCI.
Amesema wito huo ni kufuatia taarifa ya ACT Wazalendo waliyoitoa kuhusu kusinyaa kwa uchumi na kuwa serikali inapika takwimu za uchumi nchini
"Kamati kuu ni chombo cha kitaifa chenye mamlaka ya kufanya maamuzi kwa mujibu wa katiba
ya ACT kama chombo na si kama mjumbe mmoja mmoja. Jeshi la Polisi halina madaraka ya kushughulikia wa
kuingilia maamuzi halali ya vyombo
(organs) katika vyama vya siasa," amesema
Naye katibu wa itikadi, uenezi na mawasiliano wa chama
hicho Ado Shaibu amesema kamati kuu ni katibu mkuu, wenyeviti wote wa bara na
visiwani, manaibu makatibu wakuu, wenyeviti na wajumbe.
"Hivyo vigumu kwa kamati yote kuripoti kutokana na wajumbe wanatoka sehemu mbalimbali nchini lakini pia anayeweza kuwa sahihi
kutoa taarifa za kikao ni katibu mkuu au mwenyekiti wa chama," amesema
No comments:
Post a Comment