Ndemla achelewa ndege, ashindwa kuondoka...Soma habari kamili na Matukio360...#share

 Na Mwandishi Wetu

KIUNGO mshambuliaji wa Klabu ya Simba Hamis Ndemla ameshindwa  kusafiri kwenda nchini Sweden kwa ajili ya kufanya majaribio katika klabu ya AFC Eskilstuna kutokana na kukosa ndege ya kuunganisha.

Hamis Ndemla

Taarifa iliyotolewa leo na Mkuu wa Idara ya Habari na Maewasiliano wa klabu ya Simba Haji Manara amesema safari hiyo ambayo ilitakiwa kuwa leo imesogezwa mbele.

Tunapenda kuwafahamisha kuwa safari ya mchezaji wetu Hamis Said Juma Ndemla iliyokuwa ifanyike leo Jumanne imesogezwa mbele,” imesema.

Aidha emeeleza kuwa mchezaji huyo ambaye amepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya AFC Eskilstuna inayoshiriki ligi kuu nchini Sweden ,sasa ataondoka nchini siku ya Alhamis ya Novemba 9, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo imebainisha kuwa mabadiliko hayo ya safari hayataathiri muda wake wa majaribio katika klabu hiyo, ambapo atakuwa huko kwa siku 14.

Mchezaji huyo alikuwa akitokea jijini Mbeya na klbu yake ya Simba ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita walikuwa wakicheza na timu ya Mbeya City na katika mcezo huo Simba ilishinda 1-0.

Klabu ya Simba jana ilitangaza kuwa kiungo huyo amepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio nchini Swedeni.







About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search