Ndikumana azikwa Rwanda...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Rwanda
KOCHA msaidizi wa Rayon Sports ya Rwanda na aliyekuwa mume wa msanii wa filamu nchini, Irene Uwoya, mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Rwanda na kocha msaidizi wa Rayon Sport, Ndikumana Hamad Katauti (39) amezikwa jioni ya leo Novemba 15,2017  jijini Kigali, Rwanda.

Ndikumana enzi za uhai wake akiwa na mzazi mwenzake, Irene Uwoya
Hii leo Daktari mkuu wa timu ya taifa ya Rwanda, Lugemana Charles ameiambia Matukio360 kuwa amezikwa kutokana na familia yake kutaka hivyo na kwamba sababu ya kifo chake haijajulikana.

"Ndikumana amezikwa jioni ya leo kutokana na familia yake kutaka hivyo. Hivyo hatujajua sababu iliyokatisha uhai wake," amesema

Amesema awali walipendekeza  mwili wa Ndikumana ufanyiwe uchunguzi lakini familia yake imekataa.  "Familia ya Ndikumana ni ya kiislam hivyo walikataa kufanya uchunguzi kujua sababu ya kifo," amesema daktari huyo

Daktari huyo amesema hadi juzi jioni walikuwa naye kwenye mazoezi ya timu ya taifa na kwamba waliachana akiwa mzima.

"Lakini ilipofikia majira ya saa nne usiku, nilipokea taarifa ya kufariki kwa Ndikumana, nilishangaa na nikaambiwa kabla hajafa alijisiki vibaya wakampa soda, akatapika na muda akafariki,’"amesema

Mapema leo taarifa kutoka Rwanda zilisema  Ndikumana Hamad ''Katauti'' ambaye ni mume wa zamani na Baba wa mtoto wa muigizaji maarufu nchini, Irene Uwoya alifariki dunia usiku wa kuamukia leo bada ya kuugua ghafla.

Kataut alikuwa beki wa zamani wa Rayon Sports ya Rwanda  pia amewahi kuchezea timu ya soka ya Stand United ya Shinyanga wakati akitokea Cyprus.

Taarifa kutoka Kigali, Rwanda zinaeleza  kwamba alikuwepo mazoezini jana jioni na hadi anapoteza maisha alikuwa ni kocha msaidizi wa kikosi cha Rayon Sports ya Rwanda.

Mara ya mwisho alikuja nchini mwaka 2017 wakati wa Simba Day Agosti 8, akitua nchini Agosti 7 akiwa na kikosi cha Rayon ambacho kilicheza na Simba na kupoteza kwa bao 1-0.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search