NEC yarejesha wagombea tisa udiwani...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
TUME ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imewarejesha wagombea tisa wa kiti cha udiwani waliokuwa wamewekewa pingamizi na imezikataa  rufaa za wagombea sita.


Mwenyekiti wa NEC, Jaji  Semistocles  Kaijage (katikati) akiongoza kikao cha Tume kilichokuwa kinajadili rufaa za wagombea udiwani pamoja uteuzi wa Wanawake wa udiwani wa viti Maalum.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu (Z) Hamid Mahmoud Hamid na kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye ni Katibu wa Tume, Kailima Ramadhani. (Picha na NEC).

Hatua hiyo inafuatia baada ya Novemba 2 na 3, 2017, NEC kupitia rufaa ambapo  tisa waliondolewa kugombea, sita waliwekewa pingamizi na wagombea wenzao lakini pingamizi zao zilikataliwa na msimamizi wa uchaguzi na hivyo kuendelea kuwepo kwenye orodha ya wagombea na mmoja alipinga kukataliwa kugombea.

Hata hivyo, Tume baada ya kuchunguza rufaa moja ya mgombea anayepinga kukataliwa kugombea, imebaini mgombea alikuwa analalamika tu haikuwa rufaa hivyo Nec  itamjibu mgombea huyo kwa maadishi malalamiko yake.

Rufaa hizo ni mbili ziliwasilishwa na  CCM  ikipinga walioteuliwa, CHADEMA iliwasilisha rufaa kumi, saba kati ya hizo ilitaka wagombea wao walioondolewa kwenye orodha ya wagombea waresheshwe na tatu kilipinga wagombea walioteuliwa.
CUF iliwasilisha rufaa mmoja  ya mgombea wao ambaye hakuteuliwa, ACT-Wazalendo iliwasilisha rufaa mbili  za wagombea wao waliondolewa kugombea kwenye orodha ya wagombea warejeshwe na UDP iliwasilisha rufaa moja ikipinga mgombea aliyeteuliwa.

Oktoba 26, 2017 NEC ilipokea taarifa kuwa wagombea 30 kati ya 157 waliorejesha fomu za uteuzi na kuteuliwa kugombea kwenye  kinyang,anyiro cha uchaguzi mdogo wa marudio wa udiwani katika kata 43 wa Novemba 26, 2017, waliwekewa pingamizi na  wagombea wenzao pamoja na msajili wa vyama vya siasa.

Hata hivyo, baada ya pingamizi hizo, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata kwenye maeneo yanayofanya uchaguzi  walifanyia maamuzi pingamizi hizo ambapo wagombea  19  waliruhusiwa kuendelea na kampeni za uchaguzi na wagombea 11 waliondolewa kugombea kwenye nafasi za udiwani.

Sababu za Msimamizi wa Uchaguzi, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Mgombea na Msajili wa Vyama vya Siasa kuweka pinganizi ni pamoja na Mgombea kutokuwa raia wa Tanzania, hajatimiza umri wa miaka 21, hana sifa ya kuwa Mgombea wa Udiwani, hawezi kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kingereza, si mwanachama wa Chama cha Siasa, si mkazi wa kawaida wa Halmashauri anayogombea.

Sababu nyingine za Mgombea kuwekewa pingamizi ni kutiwa hatiani kwa kosa la kukwepa kulipa kodi katika kipindi cha miaka mitano kabla Uchaguzi, kutodhaminiwa na Wapiga Kura walioandikishwa katika Kata au idadi ya Wapiga Kura inayotakiwa waliomdhamini haikutimia, kutolipa dhamana ya shilingi elfu tano (5,000/=), kutokuwa na picha, kutowasilisha Tamko la kisheria, kutodhaminiwa na Chama cha Siasa kugombea Udiwani.

Zaidi ya hayo, Sababu nyingine  za Mgombea kuwekewa pingamizi ni kutotaja gharama na vyanzo vya fedha atakazotumia katika Uchaguzi chini ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya 2010, kutenda vitendo alivyokatazwa chini ya Sheria ya Gharama ya Uchaguzi, Kutorudisha fomu za uteuzi kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na Sheria, kutotoa Tamko la kuheshimu Maadili ya Uchaguzi ya Mwaka 2015 na kutokuwa na kipato halali kinachomwezesha kuishi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search