New Version:Wazazi wahimizeni watoto kupenda masomo sayansi na hesabu...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
WAZAZI wametakiwa kuwatia moyo watoto  kupenda masomo ya sayansi, hesabu na kulipa ada kwa wakati.

Baadhi ya wanafunzi  wa shule ya msingi New Version  iliyopo Kibaha kwa Mathias eneo la Msangani wakiwa katika michezo mbalimbali.

Wito huo umetolewa na mkurugenzi, Andrea Mfuko wa shule ya msingi  New Version yenye mfumo wa kingereza iliyopo Kibaha kwa Mathiasi eneo la Msangani.

Amesema kila mzazi na mlezi anatakiwa  kutobagua watoto katika mgawanyo wa kazi za nyumbani na pia kutambua wajibu  wa kuwafuatilia watoto shuleni hasa maendeleo ya masomo yanapokuwa hayaendi vizuri.

‘Matokeo ya darasa la saba ya mwaka 2017, New Version imeng’aa, imeshika nafasi ya pili kiwilaya nafasi ya tano kimkoa na nafasi ya 96 kitaifa huku ikiwa na wastani wa 205. 1765,’ amesema  Mfuko

Shule ya New Version yenye usajili namba  PW.01/7/010 mwaka 2016 katika mtihani wa taifa wa darasa la saba ilishika nafasi ya sita kiwilaya, nafasi ya 22 kimkoa na nafasi ya 702 kitaifa huku ikiwa na wastani wa 163.0714.

Mwaka 2015 ilishika nafasi ya kwanza kiwilaya, nafasi ya tano kimkoa na nafasi ya 224 kitaifa huku ikiwa na wastani wa 201.3913.

Wanafunzi  wa darasa la saba katika  shule ya msingi New Version  iliyopo Kibaha kwa Mathias eneo la Msangani wakiwa wamembeba  mmoja wa kijana aliyeongoza  katika mtihani wa kitaifa wa darasa la saba, 2017.
Mfuko amesema shule hiyo inawafundisha watoto kujitambua na kujua wajibu walionao kwa jamii inayowazinguka na taifa kwa ujumla na kwamba elimu ya mtoto ni mzazi na mwalimu iwapo kila mtu anatambua wajibu wake na kumthamini mwenzake kwa nafasi yake.

Maono yao ni kitoa elimu bora na kujenga   jamii yenye kujitambua ambayo itakuwa ni sehemu muhimu ya kutegemewa na taifa.

Kauli  mbiu ya shule hiyo ni 'Education brings self actualization' na mawasiliano yao ni 0712204476 na 0763243650


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search