Mkandarasi apewa miezi miwili kukamilisha barabara...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
mwandishi wetu
SERIKALI
Mkoani Mbeya imemwagiza mkandarasi wa kampuni ya M/s Chongging Internation
Constraction Corporation (CICO) kuwa ifikapo Januari, 2018 kukamilisha mradi wa
ujenzi wa barabara yenye urefu wa
kilomita kumi kwa kiwango cha lami
kutoka kijiji cha Lupaso hadi Bujesi.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla kulia akiwa na mkuu wa wilaya ya Rungwe katikati akitoa maelekezo kuhusu ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka kijiji cha Lupaso hadi Bujesi katika halmashauri ya Busekelo.
Mkuu
wa mkoa huo, Amos Makalla ametoa agizo hilo leo
katika ziara ya kukagua mradi huo uliopo katika halmashauri ya Busokelo unaogharimu bilioni 8.928 zilizotolewa na serikali, lengo kuboresha miundombinu ili kuharakisha ukuaji
wa shughuli za kiuchumi.
Kaimu
meneja wa wakala wa barabara (TANROAD) mkoani Mbeya, mhandisi Eliazary Rweikiza
amesema udongo tifutifu unaohifadhi maji muda mrefu ndio changamoto iliyochelewesha
ukamilikaji wa mradi huo na imewalazimu kufanya kazi kwa miezi mitatu tu kwa mwaka.
"Kwa
kweli changamoto kubwa ni hiyo kwani eneo hili la mradi utekelezaji wake ni
miezi mitatu kwa kila mwaka ambayo
Agosti na Novemba lakini miezi
mingine yote mradi unakwama kutokana na mvua nyingi zinazonyesha wilayani rungwe," amesema
Mkandarasi
wa mradi huo, Wang Cuengbao amesema
utakamilika kwa muda uliopangwa ili kusogeza huduma muhimu za
kijamii na waliingia
mkataba mwaka
2014 na TANROAD .
No comments:
Post a Comment