Polisi wakamata 106 Ubungo...soma habari kamili na Matukio360#...share
Na
Salha Mohamed
JESHI
la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limekamata watuhumiwa 106 katika kituo
kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo kutokana na uhalifu.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa
Akizunguma
leo jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa
amesema Polisi walifanya operesheni kali leo alfajiri katika kituo hicho kufuatia
ongezeko la wimbi la uhalifu unaofanyika kwa abiria na mali zao.
"Operesheni
hiyo imefanikisha kukamata watuhumiwa 106 ambapo watuhumiwa 95 walikamatwa kwa
makosa ya kubughudhi abiria, kuibia abiria, kuuza tiketi zisizo halali (bandia)
na kujivalisha sare za mawakala wa mabasi ili hali wao si mawakala wa mabasi
husika," amesema.
Amesema
watuhumiwa wote wamefikishwa katika mahakama
ya jiji.
Amesema
baada ya uchambuzi watuhumiwa 11
walibainika kuwa na kesi mbalimbali zinazoendelea ambapo wamepelekwa kituo
kikuu cha magomeni ili kuendelea na tuhuma zinazowakabili.
Mambosasa
amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Ahmed Said(21) mkazi wa Ubungo,Suleiman
Abdallah(30) mkazi wa Kinana, Ally
Shango(20)
mkazi
wa Kinana.
Wengine
ni Yusuph Okocha(25)mkazi wa Mabibo,Idd Mohamed (22) mkazi wa Ubungo, Yusuph
Chuma(22)Mkazi wa Manzese.
"Wengine
ni Baraka Makunda (31)mkazi wa Temeke, JUMA Bakabibi (38) mkazi wa Buguruni,
JUMA Badoni (22) mkazi wa Ubungo, Saladini Abdul (30)
mkazi
wa Ubungo na Rashid Juma(17) mkazi wa Ubungo.
"Msako
huu utakuwa endelevu katika stendi za Mbezi, Temeke na vituo vyote vya mabasi
ya abiria na mizigo, "amesema.
No comments:
Post a Comment