NEC yaridhia uamishwaji vituo 21 vya kupigia kura Mbweni...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Hussein Makame-NEC
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeridhia uamuzi wa kuhamisha vituo 21 vya upigaji kura
katika kata ya Mbweni, jimbo la Kawe, Kinondoni. na kwamba hatua hiyo imezingatia sheria na kanuni za uchaguzi.
Mkurugenzi
wa Uchaguzi NEC, Kailima Ramadhani akiwa na kitabu cha wageni kwenye Ofisi ya
Serikali ya Mtaa wa Malindi Estate ambayo ipo kwenye nyumba ya mmoja wa
wagombea wa Uchaguzi Mdogo wa Madiwani Kata ya Mbweni.Picha na NEC.
NEC imetoa msimamo huo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa baadhi ya wananchi na vyama vya siasa wakilalamika kuamishwa kwa vituo nane vya kupigia kura na kupelekwa katika kituo cha Polisi.
Pia kuhamishwa kwa vituo vingine 15 kutoka maeneo ya
awali jambo ambalo baadhi ya vyama
havikukubaliana na uamuzi huo.
Jana Mkurugenzi wa Uchaguzi, NEC Kailima Ramadhani akiambatana
na watendaji wengine wa Tume, walitembelea maeneo hayo na kujiridhisha mabadiliiko
ya vituo yaliyofanywa na msimamizi wa uchaguzi yamekidhi matakwa ya kisheria.
“Nimefika hapa
jimbo la Kawe kata ya Mbweni, baada ya mwananchi mmoja kunitumia ujumbe
akiniambia kuwa kuna chama kimoja kinachoshiriki Uchaguzi Mdogo wa Madiwani wa
Kata ya Mbweni kinalalamika kwamba Tume imehamisha vituo vya kupigia kura
kiholela,” amesema Ramadhani.
Amesema chama hicho kimelalamika kuwa vituo hivyo vimepelekwa
kwenye eneo la kituo cha Polisi, kwa hiyo huenda wapigakura wakanyimwa haki yao
ya kupiga kura.
Kailima amesema alipowauliza watendaji wa Manispaa ya
Kinondoni, majibu yao hayakumridhisha ndipo alipoamua kufika eneo la tukio.
“Kwanza wanalalamika kwamba vituo vilivyohamishwa ni 27,
lakini ukweli ni vituo 21, vituo hivyo vimehamishwa kwa mujibu wa Sheria kwa
sababu Novemba mosi 2017, Msimamizi wa
Uchaguzi ngazi ya Kata aliviita vyama vinne na kufanya mkutano na aliwaambia
tunavihamisha vituo hivyo kwa sababu mbalimbali.
“Sababu alizozitoa msimamizi wa uchaguzi ni kwamba vituo
vinane vilikuwa shule ya Sekondari New
Era na vituo saba 7 vilikuwa jirani na nyumbani kwa mgombea ambaye ni
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na vituo sita vilikuwa kwenye eneo la Kanisa,”
alifafanua Kailima.
Amebainisha kuwa kifungu cha 20 (2) cha Kanuni za
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura za Mwaka 2015 na Kifungu cha 21
cha Kanuni za Uchaguzi Mkuu wa 2015, vinabainisha kuwa vituo vya kupigia kura
havipaswi kuwa kwenye maeneo ya watu binafsi, kwenye maeneo ya ibada na kwenye kambi
za jeshi.
Kutokana na msingi wa kanuni hizo, Kailima alithibitisha
kuwa uamuzi wa kuvihamisha vituo hivyo kwenye maeneo hayo ambao umefanywa
na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la
Kawe ni sahihi.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya
Kinondoni, Aron Kagurumjuri amesema malalamiko kuhusu kuhamishwa
kwa vituo hivyo yalitolewa na chama kimoja kati ya vyama vinne vinavyoshiriki
uchaguzi.
Uchaguzi mdogo wa kata hiyo unafanyika baada ya mahakama
kutengua uchaguzi wa awali kutokana na ukiukwaji wa baadhi ya taratibu za uchaguzi.
Alifafanua kuwa hali halisi inaonesha kwamba kanuni na taratibu za kupigia kura, haziruhusu kuweka
kituo kwenye jengo la mtu binafsi, na
shule hiyo ambayo ilikuwa na vituo kadhaa ni shule ya mtu binafsi.
“Kwa hiyo kwa Uchaguzi huo wa mwaka 2015 kanuni hizo
zilikiukwa sasa kwa uchaguzi huu kwa sababu tunataka tufanye uchaguzi kwa
kufuata kanuni na sheria hatukutaka kuingia kwenye uvunjaji wa kanuni na
taratibu,” amesema
No comments:
Post a Comment