Serikali iwawezeshe maofisa ugani...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

SERIKALI imetakiwa kuwawezesha kifedha Maofisa Ugani wa kilimo na ufugaji ili waweza kuwafikia wakulima wengi kwa urahisi.

Mkurugenzi wa Jukwaa Huru la Wadau wa Kilimo (ANSAF) Audax Rukonge, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Cha Sokoine (SUA) Dk. Sizya Lugeye akizungumza na waandishi wahabari katika Mkutano wa Jukwaa Huru la Wadau wa Kilimo (ANSAF) ulioshirikisha wadau mbali mbali wakilimo na ufugaji, ameseam Maofisa Ugani wengi hawana nyenzo za kuwafikia wakulima.

“Hawajeweza kuwafikia wakulima wengi, kwa sababu nyenzo nyingi hawana, wanaishi bila baiskeli, pikipiki kwa hiyo wapo pale katika ngazi za vijiji, kata na wengine ngazi ya wilaya lakini hawatoki na hawajui kinachoendelea katika ngazi za chini yao,” amesema Dk. Lugeye.

Aidha ameitaka serikali kufikilia kubadili sera ya kuwa na Ofisa Ugani kila wilaya na badala yake kuwe na wataalamu wa ugani katika ngazi ya kata ambao wamewezeshwa kwa kupewa nyenzo zote zinazohitajika ili waweze kuwa watendaji wazuri.

Ameongeza kuwa serikali iongeze bajeti katika sekta ya kilimo na igawanywe katika kila wilaya.

Kwaupande wake Mkurugenzi wa ANSAF Audax Rukonge, akizungumza juu ya mkutano huo, amesema wamekutana kwa ajili ya kujadiliana kuhusu jinsi ya utoaji wa huduma za ugani kwa ubora unaostahili, ili kuendana na mbio za kuongeza tija katika uzalishaji na upatikanaji wa chakula hususani katika kipindi hiki nchi inapolenga kuwa ya viwanda.

Amesema kuwa wakulima wamekuwa wakilalamikia kuhusu ubora wa huduma kutoka kwa wagani, hivyo watatumia mkutano huo kujadili jinsi bora ya kuweza kuboresha huduma hizo ili kumsaidia mkulima kuzalisha zaidi lakini mazao yaliyo bora.

Amesema hilo litawasaidia wakulima kupata soko la ndani na katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Aidhaa mesema kuna haja ya kubadili mfumo wautoaji wahuduma za ugani kwa wakulima kwa kuweza kuweka rasilimali zakutosha katika vituo vya utoaji wahuduma hizo pamoja na kutoa elimu kwa Maofisa Ugani.


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Cha Sokoine (SUA) Dk. Sizya Lugeye akizungumza na waandishi wahabari jiji Dar es Salaam.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search