TECNO, VODACOM kuitambulisha PHANTOM 8...soma habari kamili na Matukio360..#share



 Mkuu kitengo cha mahusiano Vodacom Jackline

Phantom 8  ina  6GB RAM,Betri yake  ina uimara wa 3500 mAh za kuhifadhi chaji kwa  muda mrefu, 64 GB ROM, inayoipa simu uwezo wa  ziada wa kuhifadhi data  kufikia 2TB , Inavuta picha iliyombali kwa ukaribu bila kupoteza muonekano  halisi mara 10 zaidi ya simu za kawaida . Phantom 8 ina muundo na mtindo wa kuvutia hasa rangi yake yenye mng’ao wa almasi

Kampuni  kinara ya simu za mkononi  TECNO  imeungana na Vodacom kutambulisha toleo jipya TECNO Phantom 8, Simu hiyo iliyozinduliwa nchini Dubai imetambulishwa rasmi nchini Tanzania katika duka la TECNO SMART HUB lililopo Mlimani City mapema mwezi huu.




Akizungumza wakati wa utambulisho ,  Afisa mahusiano wa TECNO , Eric Mkomoya  amesema ‘’ TECNO tumeitambulisha rasmi Phantom 8 nchini Tanzania leo tukiwa na mshirika wetu wa matoleo ya Phantom nchini , Vodacom .Tumetengeneza  simu bora yenye hadhi, tunayofuraha kuwataarifu wateja wetu kuwa  Phantom 8  inapatikana katika Smart Hubs za TECNO na maduka yote ya Vodacom nchini.’’ Alihitimisha

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu kitengo cha mahusiano Vodacom Jackline amesema ‘’ TECNO inataraji wateja wake kufurahia matumizi ya toleo jipya la simu janja iliyopo sokoni ambayo tayari imejipatia umaarufu kwa kupokelewa vizuri  sehemu mbali mbali nchini Tanzania. Vodacom inawazawadia  meseji  300 , 5GB  za kuperuzi mtandaoni ,  na dakika 300 za kupiga mitandao yote kwa  wateja watakao nunua Phantom 8 katika maduka ya Vodacom yaliyopo nchini kote nchini

Ushirikiano baina ya TECNO na Vodacom umekua wa kudumu ambapo awali waliitambulisha Phantom 6 na 6+ sasa wanakuletea Phantom 8 inayotikisa soko ikiwa na 20MP kamera ya mbele na  12MP +13 MP  kamera zake 2 za nyuma.
Mwandishi wa habari Asia Matona alijinyakulia zawadi ya Phantom 8 kwa hisani ya TECNO na Vodacom.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search