Serikali kupima upya mashamba ya ushirika...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu
SERIKALI ipo katika mkakati wa kuandaa na kupima upya mashamba ya vyama vya ushirika mkoani Kilimanjaro


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi aliyesimama akizungumza na watendaji.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na  waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendele ya Makazi, William Lukuvi alipokuwa akijibu swali la mbunge kuhusu mpango wa serikali wa mashamba ya ushirika mkoani Kilimanjaro
 “Pamoja na mambo mengine Serikali inaanda utaratibu wa upimaji upya mashamba yote ya ushirika mkoani Kilimanjaro,” amesema Lukuvi

Amesema tayari ameshaiandikia wizara ya kilimo na pia kukutana kimazungumzo na wahusika wa wizara hiyo kwa kuwa mashamba hayo yapo chini yao.
Lukuvi amesema mchakato ukimalizika uenda mashamba hayo yakagawiwa kwa wananchi kadri inavyofaa ili kuyaendeleza.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search