Serikali kupunguza mimba za utotoni...Soma habari kamili na Matukio360...#share
Na Abraham Ntambara
SERIKALI imejipanga kupunguza
mimba za utotoni kwa asilimia 27 kwa
kipindi cha miaka mitano kinachoanzia 2017 hadi 2022 lengo likiwa ni kuhakikisha
mtoto wa kike anapata haki yake ya elimu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto wa Kike (CDF) Koshuma Mtengeti, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
Hayo yamesema leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa
Maendeleo ya watoto kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto,
Margaret Mussai wakati wa Kongamano la Mtoto wa Kike , liloandaliwa na Jukwaa la Utu wa Mtoto wa Kike (CDF) kwa
udhamini wa Shirika la Maendeleo Uswidi
( Swedish International Development Cooperative Agency-SIDA).
Mussai amesema kwa sasa serikali imeandaa mpango kazi wa
Taifa wa kotokomeza ukatili wa kijinsi kwa upande Mimba za Utoto.
“Katika Mpango huu
tumeanza kupunguza mimba kwa asilimia 27 kwa watoto na tunaamini mpango huu
utasaidia kundokana na tatizo hili”amesema
Amesema katika kutekeleza mpango huu, Serikali itashirikiana Taasisi zisizo za
Kiserikali katika kuhakikisha
wanapunguza Mimba za Watoto.
Hata hivyo , Mussai amewataka Watoto wa Kike kujitambua wenyewe kwa kujiepesha na mambo
yasio faa ambayo yatapelekea kuongezeka mimba za watoto ambapo amedai zimechangiwa
na watoto hao kujiingiza kwenye makundi yasioa faa.
Kw upande wake Mkurugenzi wa Mtendaji wa CDF Koshuma
Mtengeti, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwapatia fursa watoto wa kike
kukurana na Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Uswid ambapo watapata fursa ya kuelezea mafunzo
mbali mbali waliyopata kutokana na utekelezaji wa miradi mbali mbali ya CDF.
Amesema miradi hiyo ni pamoja na miradi ya kutokomeza, mimba
za utotoni, ndoa za utotoni, ukatili wa kijinsia na kuonesha kazi za
ujasiriamali walizozifanya ikiwa kama mafanikio ya miradi ya CDF.
“Vile vile katika kongamano hili, wanaume na wavulana wakiwa
kama mabalozi wa CDF watapata fursa ya kuelezea ni kwa namna gani wanafanya
kazi za kuelimisha jamii pamoja na vijana rika juu ya madhara ya ukatili wa
kijinsia, ukeketaji, mimba za utotoni pamoja na ndoa za utotoni ili kufikia
dhana ya Taifa ya kuleta usawa wa kiiinsia,” amesema Mtengeti.
Naye Mkurugenzi Mwandamizi kutoka SIDA Carin Jamtin, amesema
shirika lao limekuwa likitetea haki za woto kwa kuhakikisha watoto wakike na
kiume wanakuwa na haki sawa katika jamii hususani haki ya kupata elimu.
Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo Uswidi ( Swedish International Development Cooperative Agency-SIDA) Carin Jamtin, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya watoto kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii jinsia na Watoto, Margaret Mussai, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo Uswidi ( Swedish International Development Cooperative Agency-SIDA) Carin Jamtin, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya watoto kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii jinsia na Watoto, Margaret Mussai, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment