Serikali yapata sh. bilioni 1.6 mrahaba madini ya Almasi...Soma habari kamili na Matukio360...#share

Abraham Ntambara

SERIKALI imepata sh. Bilioni 1.614 kutokana na mauzo kwa njia ya mnada wa madini ya almasi ya Kampuni ya Williamson Diamonds Ltd.
Waziri wa Madini Angela Kairuki akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Madini hayo ni kiasi cha karati 39,567.96 kilichozalishwa na Kampuni hiyo kwa ruhusa ya serikali na kuomba wauze.

Serikali ilikubali na wataalamu wa serikali walithaminisha almasi hizo na kupata thamani ya awali ya Dola za Marekani 8,191,644.99 na mrahaba wa awali ukalipwa Dola za Marekani 491,498.70 na ada ya ukaguzi Dola za Marekani 81,916.45 na hivyo serikali kupata Dola za Marekani 573,418.15 sawa na sh.bilioni 1.288.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Slaam Waziri wa Madini, Angela Kairuki, amesema madini hayo yalisafirishwa Oktoba 20, 2017 kwenda nchini Ubelgiji na kuuzwa jana chini ya usimamizi wa maofisa wa Serikali.

“Oktoba 20,2017 almasi hizo zilisafirishwa kwenda Ubelgiji na serikali ilituma maofisa wake kusimamia uuzwaji wa almasi hizo, ziliuzwa kwa njia ya mnada jana, almasi hizo zilikuwa kwa Dola za Marekani 10,261,227.76. Thamani hii ni sawa na asilimia 20.16 kulingana na thamani ya usaminishaji wa awali,” amesema Kairuki.

Amesema kutokana na ongezeko hilo baada ya almasi hizo kuuzwa, serikali itapata mrahaba zaidi ambao ni wa mwisho (Final royalty) kiasi cha Dola za Marekani 124,174.97 na ada ya ukaguzi Dola za Marekani 20,695.83 ambayo jumla yake ni Dola za Marekani 144,870.80 sawa n ash. Milioni 325.525.

Hivyo amesema jumla ya mapato yote kutokana na mauzo hayo ni Dola za Kimarekani 718,288.95.

Aidha amesema baada ya serikali kuzuia mzigo wa almasi wa kampuni hiyo zilizokuwa zisafirishwe Antwerp-Ubelgiji Agosti 31, 2017 ili kujiridhisha  kuhusu thamani halisi ya almasi hizo bado upo  na taratibu za kuthibitisha thamani halisi zinaendelea.

Katika hatua nyingine Waziri Kairuki amesema usiku wa kuamkia Oktoba 29, 2017 katika eneo la Kiabakari, serikali ilikamata  sampuli za miamba ya madini ya dhahabu takribani kilo 600 zilizokuwa zinasafirishwa na Kampuni ya wachina inayoitwa ZEM (T) Ltd bila vibari kutoka wizara ya madini.


Hivyo serikali imeamua kuwapeleka mahakamani ili sharia ichukue mkondo wake.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search