NBS: Mfumuko wa bei washuka...Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

MFUMUKO wa bei nchini kwa mwezi Oktoba, 2017 umeshuka hadi kufikia asilimia 5.1 ikilinganishwa na asilimia 5.3 ilivyokuwa mwezi Septemba, 2017.
Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya, amesema hiyo inamanisha kuwa, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Oktoba, 2017 imepungua ikilinganishwa na kasi ya ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi Septemba, 2017.

Aidha amesema kushuka kwa Mfumuko wa Bei wa mwezi Oktoba, 2017 kumechangiwa na kushuka kwa bei za bidhaa ya baadhi za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Oktoba, 2017 zikilinganishwa na bei za mwezi Oktoba 2016.

“Baadhi ya bidhaa za vyakuli zilizochangia kupungua kwa Mfumuko wa Bei ni pamoja na, unga wa mtama kwa asilimia 2.6, samaki kwa asilimia 7.1, matunda kwa asilimia 2.7, mbogamboga kwa asilimia 7.4, maharage kwa asilimia 2.9,viazi kwa asilimia 14.4, na karanga kwa asilimia 7.8,” amesema Ruyobya.


Ruyobya  ameongeza kuwa Mfumuko wa Bei nchini una mwelekeo unaofanana na baadhi ya nchi nyingine za Afrika Mashariki ambapo nchini Kenya Mfumuko wa Bei wa mwezi Oktoba, 2017 umeshuka hadi asilimia 5.72 kutoka asilimia 7.06 mwezi Septemba, 2017 na nchini Uganda umeshuka hadi asilimia 4.8 mwezi Oktoba, 2017 kutoka asilimia 5.3 mwezi Septemba, 2017.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search