Serikali yasajili machapisho 109...Soma habari kamili na Matukio360../#share

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imesema hadi kufikia Oktoba 31, 2017, ambayo ni siku ya mwisho ya utoaji wa leseni kwa machapisho ya zamani, Idara imetoa leseni za machapisho 109 na kati ya hayo 85 ya zamani na 24 mapya.

Mkurugenzi Mkuu, Idara ya Habari -Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abbasi.

Aidha imepiga marufuku kuanzia sasa kutoa machapisho ya magazeti na vijarida kwa watu binafsi na taasisi ambazo hazikukamilisha taratibu za usajili na kupatiwa leseni kwa muda uliokuwa umewekwa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo na Mkurugenzi Mkuu, Idara ya Habari -Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abbasi, imesema  kuwa utoaji wa leseni kwa machapisho yaliyosajiliwa nchini ni utekelezaji wa matakwa ya kifungu cha 5(e) cha sheria hiyo. 

“Serikali kupitia Idara ya Habari (Maelezo) inautaarifu umma kuwa juzi , oktoba 31, 2017, imekamilisha awamu ya kwanza ya utoaji wa leseni za uchapishaji wa magazeti na majarida yaliyokuwa yamesajiliwa awali kabla ya kuanza kutumika kwa sheria mpya ya Huduma za Habari No. 12 ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2017,” imesema.

Aidha imesema baada ya kumalizika kwa kipindi hicho ambacho kilikuwa ni muda wa nyongeza baada ya agizo la awali kumalizika Oktoba 15 mawa huu, omeeleza kuwa watu binafsi na taaasisi ambazo hazikukamilisha taratibu husika ndani ya kipindi hicho kuwa kwa sasa hawataruhusiwa tena kuendelea kutoa machapisho hayo hadi watakapo pata leseni Mpahya.

Mbali na hilo, imesema kuwa ni muhimu kufahamu kuwa ni kosa la jinai kuchapisha gazeti, jarida au machapisho mengine yaliyoainishwa kwa mujibu wa sheria bila kuwa na leseni, isipokuwa kwa idhini maalumu tu, kwani kwa mujibu wa kifungu cha 50(2) (a) cha Sheria ya Huduma za Habari, 2016, ikithibitika kutendeka kosa hilo adhabu ni faini kati ya sh. Milioni 5 hadi 10, kifungo cha miaka mitatu hadi mitano au vyote kwa pamoja.

Aidha idara imesema itaendelea kutoa huduma za kutoa leseni mpya kwa machapisho ya zamani na mapya.

Agosti 23, 2017 serikali ilitangaza kufanya usajili mpya na utoaji wa leseni kwa magazeti na vijarida ambapo ilitoa muda wakukamilisha zoezi hilo kuwa Oktoba 15, lakini baadaye muda huo uliongezwa hadi Oktoba 31, 2017.


Taarifa ya Serikali



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search