Mali za meneja wa Diamond kupigwa mnada...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na mwandishi wetu
KAMPUNI ya Tiptop
Connection Company Limited inayomilikiwa na Hamis Shaban Taletale ‘Babu Tal’
ambaye ni Meneja wa Diamond Plutnam na Idd Shaban Taletale, iko hatarini
kupigwa mnada kwa kushindwa kulipa fidia ya milioni 250.
Msanii na mkurugenzi wa kampuni ya, TipTop Conection Ltd, Hamisi Shabani 'Babu Tale'
Tayari kampuni ya
udalali ya Yono Auction Mart & Co Ltd imewapa siku 14, Babu Tale na nduguye
kama wakurugenzi wa kampuni hiyo kutaja
mali za kampuni hiyo, au wao wenyewe wawe wamelipa pesa hizo ndani ya muda huo.
Hatua hiyo ya Yono ni utekelezaji wa amri ya
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam iliyoamuru kampuni hiyo kumlipa fidia ya
milioni 250 Mhadhiri wa Dini ya Kiislama, Sheikh Hashim Mbonde.
Mahakama Kuu,
Februari 18, 2016 iliamuru kampuni hiyo kumlipa fidia hiyo Sheikh Mbonde kwa
kutumia kazi zake za masomo na mahubiri kibiashara bila ridhaa wala makubaliano
naye, jambo ambalo ni kinyume cha Sheria,
Baada ya hukumu hiyo,
Sheikh Mbonde alifungua maombi ya utekelezaji ndipo Juni 9,2017 Naibu Msajili
wa Mashauri aliwaamuru Babu Tale na ndugu yake waweke wazi mali za kampuni
hiyo, au walipe fidia hiyo.
Pia katika uamuzi huo
Naibu Msajili Mashauri aliamuru kuwa kama watashindwa kutaja mali hizo wala
kulipa wenyewe fidia hiyo basi mali zao zitapigwa mnada na kama hawana mali
basi watafungwa jela kama wafungwa wa kesi ya madai.
Leo Sheikh Mbonde
amesema tayari wameshawapelekea kina
Babu Tale taarifa hiyo, na kwamba taarifa hiyo ilikabidhiwa na Meneja Masoko wa
Yono, Kene Mwankenja, kwa Kaimu Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mpakani
iliyopo Kata ya Kwembe, wilaya ya Ilala, John Wilson, ili awafikishie.
Katika kesi ya msingi namba 185 ya mwaka 2013,
Sheikh Mbonde alikuwa akidai fidia ya jumla ya milioni 750 kwa kutumia kazi
zake za mihadhara kibiashara bila idhini yake kinyume cha makubalino.
Sheikh Mbonde alikuwa
anaiomba mahakama imwamuru mdaiwa (Tip Top Connection) imlipe fidia ya jumla ya
Smilioni 700 ikiwa ni fidia ya hasara na
kuwa faida aliyotarajia kuipata kutokana na mauzo ya kazi zake hizo na milioni 50.
Kwa mujibu wa hati ya
madai na kwa mujibu ushahidi wa upande madai wakati wa usikilizwaji, Juni 6,
2013 Sheikh Mbonde aliingia makubaliano na kampuni hiyo, kutumia kazi zake za
mawaidha, kwa kuzalisha, kurekodi na kuzisambaza.
Walikubaliana
kwamba kampuni italipia gharama za kurekodi masomo na mafundisho ya mihadhara
yake, kumnunulia gari, kumjengea nyumba na kuzitangaza kazi zake kupitia vyombo
vya habari.
Pia
walikubaliana kuwa baadaye wangeingia makubaliano ya kugawana faida ambayo
ingepatikana kutokana na mauzo ya kazi hizo na siku hiyohiyo ilimlipa milioni 2
na ikamnunulia kanzu na kofia kwa
maandalizi ya kurekodi mkanda wa video wa kazi hizo katika mfumo wa DVD.
Baadaye
katika tarehe tofauti na katika misikiti
tofauti kampuni hiyo ilirekodi masomo mbalimbali aliyokuwa akiyatoa na baada ya
kukamilisha kurekodi masomo saba, kampuni hiyo ilimkatia mawasilino.
Baadaye
mmoja wa maafisa wa mdaiwa, Adam Waziri alimweleza mdai kuwa wamesitisha mpango
wa kuendelea na kazi hiyo na kwamba mdai hakuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana
na maelezo hayo.
Hata
hivyo Agosti 9, 2013, wakati mdai
akiendesha mhadhara Bahi Dodoma, alibaini kuwa DVD za masomo yake zilikuwa
zikiuzwa sokoni Dodoma na katika mikoa
mbalimbali kama vile Mbeya, Tanga na Dar es Salaam, bila ridhaa yake wala
makubalino.
DVD
hizo kwa mujibu wa hati hiyo zilikuwa ni za masomo mbalimbali aliyokuwa
ameyatoa na kwamba makava ya DVD hizo zilikuwa na nembo na namba za simu, za
maafisa wa mdaiwa.
No comments:
Post a Comment