Simba yamruhusu Ndemla kwenda Sweden....soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu


KIUNGO mshambuliaji wa Klabu ya Simba Hamis Ndemla amepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya AFC Eskilstuma inayoshiriki ligi kuu nchini Sweeden.

Hamis Ndemla

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na mkuu wa Kitengo cha Habari wa klabu hiyo, Haji Manara imesema Ndemla anatarajiwa kuondoka nchini kesho Novemba 7, 2017.  Atakuwa kwenye majaribio  kwa siku 14 nchini humo. 




"Klabu ya Simba inayofuraha kutangaza kuwa mchezaji wake Hamis Said Juma (Ndemla) amepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa nchini Sweeden.

Klabu ya Simba inaamini Ndemla atafanya vizuri na kufuzu majaribio hayo. Klabu ya Simba inaendelea kuamini katika kutoa nafasi kwa wachezaji wake kwenda nje kujaribu bahati ya kucheza soka la kulipwa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search