Kiungo Mbeya City apanga kuinyoosha Yanga...Soma habari kamili na Matukio360..#share


NA MWANDISHI WETU

KIUNGO  mshambuliaji wa Mbeya City,Mohamed  Mkopi, ameapa kuiua Yanga kama atapata nafasi ya kucheza pambano kati ya timu hizo ambao umepangwa kupigwa kwenye Uwanja wa Uhuru,Dar es Salaam.

Kikosi cha Timu ya Mbeya City

Mkopi amefanikiwa kuifungia Mbeya City bao moja katika Ligi Kuu Tanzania Bara inayoendelea sambamba na kutoa pasi tano zilizowezesha kupatikana kwa mabao.

Mohamed amesema ameifatilia a Yanga kwenye michezo yake zaidi ya mmoja na kubaini  mapungufu yao ambayo anaamini  atayatumia kuwafunga  kama atapata nafasi yankucheza mchezo kati ya timu hizo.

“Siwezi kuwabeza kwani wana timu nzuri yenye wachezaji wazuri  ambao wanabadirika kutokana na aina ya mchezo, lakini kama nitapata nafasi ya kucheza hawataweza kunizuia kutimiza lengo langu,” amesema.

Amesema kuwa msimu huu amepania kurudi katika ubora wake mara baada ya uliopita kuwa nje ya uwanja  baada ya kufungiwa na Shirikisho la Soka Tanzania(TFF )kutokana na usajili wake kukiuka taratibu.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search