SUMATRA : Disemba mwisho kuzungumza siasa, dini, biashara ndani ya basi

Na mwandishi wetu

MAMLAKA ya usimamizi wa usafri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) inatarajia kuwa Disemba, 2017 itakuwa  mwisho kwa abiria kuzungumza masuala ya siasa, dini na kufanya biashara wawapo safarini.

Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA),Gilliard Ngewe

Agizo hilo limezidi kusisitizwa  leo na ofisa elimu wa Sumatra, Nicolas Kinyelili na kwamba kanuni ya leseni ikikamilika zoezi hilo litaanza mara moja.

"Duniani kote hakuna mahala watu wanapomaliza uchaguzi wanaendelea na siasa, mambo ya mazungumzo ya dini yanamahala pake na hata biashara," amesema Kinyelili

Amesema kanuni mpya za leseni ya usafirishaji zinakaribia kukamilika na zimezingatia matakwa na taratibu za usafirishaji. " Uenda Disemba, 2017 zikaanza kazi.'' amesema

Hivi karibuni mkurugenzi mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe amenukuliwa akisema dereva na abiria atakayebainika kufanya vitendo hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na kwa wasafirishaji watanyanganywa leseni.

Agizo hilo linakuja baada ya hivi karibuni kudaiwa kuwapo kwa mvutano wa kupinga kanuni mpya kati ya Sumatra na chama cha wamiliki mabasi yaendayo mikoani (Taboa) na  wa usafiri Dar es Salaam (UWAMADAR)

Taboa na Uwamadar wamedai kuwapo katika malumbano na Sumatra kuhusu kanuni  hizo mpya  zinazotarajia kutumika hivi karibuni baada ya mchakato wake kukamilika.

Mkurugenzi wa huduma za sheria wa Sumatra, Tumaini Silaa amesema Sumatra ipo kwa ajili ya kuhakikisha wadau wote wa usafiri wanapata haki sawa.
Amesema kanuni mpya bado zipo katika mchakato na kwamba haziwezi kuanza hadi hapo wadau wote watakapokubaliana.

‘Kimsingi mambo haya ya  kanuni mpya haziwezi kuanza kabla ya kujadiliana na wadau wote wa usafiri, hivyo naamini hili haliwezi kuwa jambo kubwa sana na litapatiwa mfumbuzi,’ amesema.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search