Kesi dawa za kulevya Masogange kuanza kujitetea..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki

JANUARI 17, 2018 Agnes Gerald ‘Masogange’ ataanza kujitetea dhidi ya shtaka la kutumia dawa za kulevya linalomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Mnogeshaji, Agnes Gerald 'Masogange'

Mshtakiwa huyo ambaye ni mnogeshaji wa video (Video Qeen),alipaswa kuanza kujitetea leo   kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri  lakini imeshindikana kwa sababu hajaandaliwa.

Wakili Nehemia Nkoko ameeleza kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya Masogange kuanza kujitetea lakini hawakumuandaa kutokana na kupata msiba

Hakimu alikubaliana na hoja hiyo na kuiahirisha hadi Januari 17,2018 atakapoanza kujitetea.

Hatua hiyo imefikiwa mara baada ya Hakimu Mashauri kumuona mshtakiwa huyo kuwa ana kesi ya kujibu na kwamba anapaswa kujitetea na kuwaita mashahidi wa kumsaidia ambapo anatarajia kuwaita mashahidi watatu.

Masogane anatetewa na Mawakili  Nehemia Nkoko na Ruben Simwanza. Kesi hiyo inaendeshwa na  Wakili wa Serikali, Costantine Kakula ambaye kwa upande wao  waliwaita mashahidi watatu wa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wao na kuufunga.

 Masogange anakabiliwa na mashtaka mawili ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Anadaiwa kufanya makosa hayo chini ya kifungu cha 18 (a) cha sheria ya kupambana na dawa za kulevya namba 5 ya mwaka 2015.

Katika kesi hiyo namba 77 ya mwaka 2017,
Masogange anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14,2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam  alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).

Pia anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14,2017  alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search