Sumatra, Taboa wakanusha mgomo, wakili kulumbana ...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

MAMLAKA YA Usimamizi wa usafri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) na Chama cha wamiliki mabasi yaendayo mikoani (Taboa) wamekanusha kuwapo kwa mgomo wa usafirishaji  unaoelezwa kuwapo kuanzia kesho.
Wadau wa Usafirishaji, kutoka kulia ni Issa Nkya Mweka Hazina Taboa, Kismat Dhalla Mwenyekiti UWADAR, Tumaini Silaa Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Sumatra wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Pia wamekili kulumbana katika kanuni na sheria mpya zinazotarajia kutumika hivi karibuni baada ya mchakato wake kukamilika.

Leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa wadau wa usafirishaji UWADAR, Kismat Dhalla amekanusha taarifa zilizozagaa kwenye mitandao kuwapo kwa mgomo huo na kwamba taarifa hizo ni uongo

‘Hakuna mgomo wowote uliotangazwa na wasafirishaji(Taboa)  hivyo wadau wa usafirishaji waendelee na shughuli zao kama kawaida,’ amesema Dhalla.

Dhalla amesema pamoja na mambo mengine Jumatano wiki watakaa na Sumatra kujadili masuala kadhaa ikiwamo kanuni na sheria mpya za usafirishaji.

Mweka hazina wa Taboa, Issa Nkya amesema wapo kwenye msuguano na Sumatra kuhusu kanuni na sheria hizo na kwamba watazipatia ufumbuzi muda si mrefu.

Mkurugenzi wa huduma za sheria wa Sumatra, Tumaini Silaa amesema Sumatra ipo kwa ajili ya kuhakikisha wadau wote wa usafiri wanapata haki sawa.

Amesema sheria na kanuni mpya bado zipo katika mchakato na kwamba haziwezi kuanza hadi hapo wadau wote watakapokubaliana.

‘Kimsingi mambo haya ya kisheria na kanuni mpya haziwezi kuanza kabla ya kujadiliana na wadau wote wa usafiri, hivyo naamini hili haliwezi kuwa jambo kubwa sana na litapatiwa mfumbuzi,’ amesema.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search