Sweden yaituliza Italia, Boffuon ang'oka ....soma habari kamili na Matukio360...#share

TIMU ya soka ya Sweden imefuzu fainali za kombe la dunia za mwaka 2018 nchini Urusi baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana na Italia.


Wachezaji wa Sweden wakishangilia kufuzu kombe la Dunia mwaka 2018 mara baada ya kutoka suluhu na Italia.

Matokeo haya yanaifanya Sweden kushiriki mashindano haya tangu mwaka 2006 waliposhiriki kwa mara ya mwisho.

Italia ambao ni mabingwa mara nne wa kombe la dunia imeshindwa kufuzu ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 1958.


Hii ina maana kwamba Itali ‘Azzurri’ watayakosa mashindano hayo kwa mara ya pili tokea kuanzishwa, mara ya kwanza ilikua mwaka 1930.

Kiungo Jakob Johansson wa Sweden aliyefunga goli katika mzunguko wa kwanza alikuwa katika kiwango bora na kuwadhibiti vyema Italia katika uwanja wa San Siro.

Wengi walitaraji Italia kushinda mchezo huu kwa sababu lukuki ikiwemo historia sambamba na kucheza nyumbani.

Italia walitawala mchezo kwa asilimia 75 na kupiga mashuti 27 lakini bahati haikuwa upande wao.

Nusura mshambuliaji Stephan El Shaarawy aandike bao lakini juhudi za mlinda mlango wa Sweden Robin Olsen zilizima ndoto yake.

Kufuatia kuondolewa huko kipa mahiri wa taifa hilo, Gigga Boffuon amejiudhuru kuchezea timu hiyo.

Baadhi ya wachezaji wa Italia mara baada ya mechi na Sweden kumaliza kwa suluhu usiku wa kumakia leo



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search