Zaidi ya watu 400 wafariki...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na mwandishi wetu
ZAIDI ya watu 400 wamefariki na wengine zaidi ya 7,000 wamejeruhiwa katika
tetemeko kubwa kukumba eneo la mpaka wa Iran na Iraq. Jitihada kubwa za uokoaji
zinaendelea.
Askari wakiokoa baadhi ya watu waliofunikwa na majengo
Makundi
ya uokoaji yanatafuta manusura waliokwamwa ndani ya vifusi vya majengo
yaliyoporomoka.
Tetemeko
hilo la ardhi la incha 7.8 ndilo baya zaidi kutokea duniani mwaka huu.
Watu
wengine waliouawa walikuwa kwenye mji ulio magharibu mwa Iran wa Sarpol-e-Zahab
ulio umbali wa kilomita 15 kutoka mpaka na sehemu zingine za mkoa wa
Kermanshah.
Hospitali
kuu wa mkoa huo iliharibiwa vibaya na kusababisha ikubwe na matatizo ya
kuwahudumia wagonjwa.
Mwanamke
mmoja na mtoto waliondolewa kutoka kwa vifusi wakiwa hai kwenye mji huo, kwa
mujibu wa vyombo vya habari nchini Iran.Majengo
mengi katika mji huo yanaonekana kuporomoka
Huduma
za maji na umeme zimekatwa katika miji mingine na baada ya majengo kuporomoka
watu walilazimika kulala nje kwenye baridi.
Shirika
moja la utoaji misaada lilisema kuwa watu 70,000 wanahitaji makao baada ya
tetemeko hilo, na kuna ripoti kuwa maelfu ya watu huenda wakalala nje kwa usuku
wa pili.
Maafisa
nchini Iran wanasema kuwa watu 413 wameuawa nchi humo. Baadhi ya wanajeshi na
walinzi wa mpaka ni kati ya wale waliouawa.
Nchini
Iraq watu 9 waliuawa kwa mujibu wa msemaji wa shirika la msalaba mwekundu.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini humo ilisema kuwa watu 500 walijeruhiwa huko
na tetemeko hilo lilisikika huko Irbil, Sulaimaniya, Kirkuk, Basra na mji mku
Baghdad.
Maporomoko
yamefanya vigumu kwa waokoaji kufika maeneo ya vijijini na kuna hofu kuwa
huenda bwawa lilo huko likapasuka baada ya kuharibiwa na tetemeko hilo. Watu
wanaoishi karibu wametakiwa kuhama
No comments:
Post a Comment