Tanzania yapokea bilioni 435.7...Soma habari kamili na Matukio360...#share


Salha Mohamed

WIZARA ya Fedha na Mipango imepokea msaada wa bila riba wa bilioni 435.79 kutoka serikali ya Sweden



Leo jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu Wizara hiyo, Doto James amesema wamesaini msaada wa kibajeti bilioni 53.20, msaada wa kusaidia mpango wa elimu bilioni 235.40

Pia taasisi ya Global pertinaship imetoa milioni 94.8 kama msaada wa marekebisho ya kusaidia mpango wa kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

"Wametupa msaada na wala simkopo haliwezi kuwa sehemu ya deni la taifa, wametusaidia kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti yetu,"amesema Katibu Mkuu huyo

Amesema kwa mwaka wafedha  2017/2018 serikaliya Sweden itatoa msaada wa kibajeti wa bilioni 53.20 

Amesema misaada hiyo wameichambua na kwamba imetimiza matakwa ya sheria ya misaada ya mikopo na dhamana suraya 134.

Amesema sekta ya elimu inapaswa kusimamiwa kikamilifu kwani tangu elimu bure ianze kume kuwa na ongezeko la wananfunzi kujiunga na shule hivyo kupitia msaada huo wameboresha mazingira ya kusomea.

Amesema katika miaka miwili, sekta ya elimu imekuwa na maendeleo na kuwa shule 361 katika halmashauri 129 zimejengwa na zingine kukarabatiwa na vyuo 17 vimekarabatiwa na kufungwa kopyuta 260, magodoro 6730 na viti vya kukalia 1976.

"Sekta ya elimu inachukua asilimia 18 ya fedha za bajeti na ni sekta inayoongoza kwa kutengewa bajeti kubwa na serikali,"amesema.
    





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search