EAC yatakiwa kuunga mkono sekta binafsi…Soma habari kamili na Matukio360...#share


Na Abraham Ntambara

SERIKALI za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zimetakiwa kushirikiana na sekta binafsi ili kufanikisha mapinduzi ya viwanda.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Baraza la wafanybiashara na Wajasiliamali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Dar es Salaam.

Ombi hilo limetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa IBM holdings, Tanzania Felix Mosha katika ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa Baraza la Wafanyabiashara na Wajasiliamali wa EAC.

“Ushirikiano wa sekta binafsi na serikali za EAC utafanikisha kuleta mapinduzi ya viwanda,” amesema Mosha.

Aidha amezitaka kuwekeza katika miundombinu kama ya barabara, reli na umeme na teknolojia ili kuwasaidia wafanyabiashara katika kuwarahisishia shughuli zao.

Ameongeza kwa kuomba kuondolewa kwa vikwazo mipakani, laikini pia kuhakikishiwa usalama kwani hakuna mfanyabiashara wala mwenyekezaji anayeweza kuwekeza mahali pasipo na usalama.

Kwa upande wake Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa mgeni rasmi, amesema serikali itahakikisha inashirikiana na wafanyabiashara kwa kuwahakikishia usalama lakini pia kusimamia sheria.

Pia amesema itaboresha miundombinu ya barabara, reli na umeme ili kusaidia katika kuongeza uzarishari pamoja na upatikanaji wa soko.

Aidha amewataka wadau katika mkutano huo kujadili changamoto mbalimbali zinazokabili sekta hiyo katika EAC ili waje na mapendekezo ambayo yataboresha katika kusaidia sekta ya viwanda.

Aliwahakikishia kuwa serikali itaendelea kushirikiana kwa nguvu zote katika yale yote yaliyokatika bakubaliano ndani ya Jumuiya.

Lengo la mkutano huo ni kujadili changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa EAC na jinsi ya kuzitatua ili kusaidia katika mapinduzi ya viwanda.






About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search