Uamuzi kesi ya Mobeto dhidi Diamond kesho...soma habari na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa Watoto kesho inatarajiwa kutoa uamuzi kama kesi iliyofunguliwa na mwanamitindo, Hamisa Mobeto dhidi ya mwanamuzi, Nassib Abdul 'Diamond Platnum' itupiliwe mbali ama la.

 Msanii wa muziki, Nassib Abdul 'Diamond Platnum

Uamuzi huo  unatarajiwa kutolewa na Hakimu Devotha Kisoka wa mahakama hiyo. Hakimu Devotha atatoa uamuzi huo baada ya kusikiliza hoja za pande hizo mbili husika  kutokana na msanii Diamond kuwasilisha pingamizi dhidi ya kesi hiyo iliyofunguliwa na Mobeto.

Kwa mujibu wa pingamizi lililowasilishwa na  Diamond  mahakamani hapo anadai kuwa  kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi.  Hoja ambayo ilipingwa na Mobeto.

Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine anaomba matunzo ya mtoto waliozaa na msanii Diamond.

Mobeto  anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi. Alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys.

Kupitia hati hiyo ya madai, Mobeto  anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.


Diamond aliwasilisha hati ya majibu hayo kinzani akipinga maombi hayo ya Mobeto  akidai  gharama anazodai kulipwa kwa mwezi ya milioni 5 kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa  na hawezi kuzimudu. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search