'UPDATES' Mtoto wa Chacha Wangwe alipa faini aachiwa huru ...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abdulrahim Sadiki

BOB Chacha Wangwe ambaye ni  mtoto wa mwanasiasa marehemu Chacha Wangwe, amenusuruka kifungo cha mwaka mmoja na nusu jela baada ya  kulipa faini ya milioni 5.


Mapema leo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimuhukumu BOB Chacha Wangwe kulipa faini ya milioni 5  ama kutumikia kifungo cha mwaka mmoja na nusu jela.

Ni baada ya kupatikana na hatia katika shtaka la kuchapisha taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii.

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alitoa hukumu hiyo leo baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi sita wa  upande wa mashtaka, vielelezo 5 na utetezi wa mshtakiwa mwenyewe.


Amesema kuwa Mei 7, 2016 askari polisi walipata taarifa ya chapisho la mtoto huyo wa Chacha Wangwe, Bob ambapo walianza kumfuatilia na kumkamata kisha walichukua simu na kuipeleka maabara ya Polisi ili kuikagua.

Bob hukupinga kuandika maneno hayo lakini umedai kuwa hakuyachapisha katika mtandao wa kijamii bali yalikuwa ni siri kwenye akaunti yake.

Hakimu Shaidi alisema kuwa wakati wa ushahidi imeelezwa kuwa simu yake ilipokaguliwa ilionekana ilitumika kuchapisha ujumbe huo kwa jamii na watu walijibu, ikiashiria ujumbe uliwafikia.

Nidhahiri ulikuwa na nia ya kuchapisha taarifa hiyo, kueleza kile ambacho ulikiona sahihi kama ingekuwa ni ujumbe wako binafsi basi polisi wasingeweza kukutafuta, na watu wasingekujibu.

Hakimu Shahidi alisema kutokana na hatua hiyo Bob alokutwa  na hatia chini ya kifungu cha 16 cha sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015.

Bob aliomba apunguziwe adhabu kwa sababu ni mwanafunzi wa masomo ya sheria, pia ni kijana mdogo na ni kosa lake la  kwanza kulitenda.

Hakimu Shaidi alisema anakubaliana na hoja za Bob, kwani mahakama inamuona bado ni mdogo na anapaswa kufanya mambo mengi mazuri katika jamii.


Pia amesema kama yeye ni mwanafunzi wa masomo ya sheria anapaswa kufanya mambo mema katika jamii vitu ambavyo wengine watamuiga.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search