Mugabe ang'olewa urais Zimbabwe ...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu

EMERSON Mnangagwa ametangazwa kuwa rais wa mpito nchini Zimbabwe kwa tiketi ya chama cha ZANU-PF.
Emerson Mnangagwa

Mnangagwa alikuwa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo chini ya Rais Robert Mugabe.

Kwa mujibu wa taarifa ya chama cha ZANU-PF, inasemama Mnangagwa amefanywa kuwa rais wa mpito.

Hivi karibuni Mnangawa mwenye umri wa miaka 75 alifutwa kama makamu wa rais kutokana na kile serikali ilisema kuwa kutokuwa mtiifu.

Kufutwa kwake kulionekana kama nia ya kumwezesha mke wa rais Mugabe, Grace kufuata nyayo za mumewe na kuwa kiongozi wa Zimbabwe.

Awali alikuwa ametoa wito kwa mumewe kumfuta makamu wa rais.

Mnangagwa ambaye ni mkuu wa zamani wa ujasusi amekuwa mtu ambaye alitarajiwa kumrithi rais Mugabe 93.


Kufutwa kwake kulimaanisha kuwa Grace Mugabe anatarajiwa kuteuliwa kuwa makamu wa rais wakati wa mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi ujao.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search