Viongozi ACT wahojiwa kwa saa sita...Soma habari kamili na Matukio360..#share


Na Abraham Ntambara

VIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo wamehojiwa  na Jeshi la Polisi katika Kituo cha Makosa ya kifedha, Kamata jijini Dar es Salaa  kwa takribani saa sita.


Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Yeremia Maganja  akizungumza na waandishi wa habari baada ya mahojiano na Jeshi la Polisi katika Kituo cha Makosa ya kifedha, kamata jijini Dar es Salaa.

Waliohojiwa ni Katibu Mkuu wa Chama hicho  Doroth Semu na Mwenyekiti Yeremia Maganja kwa niaba ya Kamati Kuu ya chama ambao walianza kuhojiwa saa 3:30 asubuhi hadi saa 9:15 alasiri.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mahojiano hayo, Maganja amesema wamehojiwa kuhusiana na kamati kuu kuchambua na kuiandaa taarifa ya  kina ya Takwimu za Serikali juu ya hali ya uchumi wa nchi kusinyaa kinyume na Kifungu cha 37(5) ya Sheria ya Takwimu 2015.

"Kwa kuwa tumeambiwa tunatuhumiwa, basi tumekubaliana na tumetoa maelezo yetu, na tumemueleza mwakilishi wa DCI kwamba wajumbe wa Kamati Kuu wanatoka nchi nzima na ni wahali ya kawaida wa maisha ya kawaida hatuwezi kukusanyika kwa siku mbili tatu wakaweza kufika kwa hiyo wametuelewa kwamba ni vigumu kuwakusanya kwa wakati mmoja ndani ya siku nne wakawa wamefika," amesema Maganja.

Aidha amesema kutokana na ugumu wa kuwakusanya wajumbe wote wa kamati na kuripoti polisi kama witoulivyokuwa ukiwataka wameacha namba za simu na majina ya wajumbe wa kamati kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ili kama watawahitaji wawatafute.

Maganja ameongeza kuwa wametakiwa kuripoti tena kituoni hapo Novemba 26, 2017 kwa ajili ya kujua hatua nyingine zaidi zitakazofuata.

Awali Kiongozi wa Chma hicho Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufika katika kituo hicho cha Makosa ya Kifedha cha Kamata akitokea kituo cha Polisi Chang'ombe majira ya saa 5 asubuhi alipokuwa ameripoti kwa  ajili ya kujua hatma yake ikiwa atafikishwa mahakamani au vinginevyo, amesema kuwa ametakiwa kurudi kituoni hapo November 17,2017.
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka kituo cha polisi cha Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Pia amesema anatakiwa kuripoti kesho polisi katika Kituo cha Makosa ya kifedha, kamata jijini Dar es Salaa kwa ajili ya mahojiano na DCI

"Chang'ombe wanasubiri hati ya mashtaka kutoka kwa DPP  na  kama upelelezi upo tayari wataangalia uwezekano wa kunipeleka mahakamani, lakini pia kesho nimetakiwa kuripoti hapa," amesema Zitto.


Zitto ameongeza kuwa ikiwa suala hilo litapelekwa mahakamani itakiwa ni kesi ya kwanza ya namna hiyo katika historia nchini  kuhusu masuala ya Takwimu ya Taifa kupelekwa mahakamani.

Ameongeza kuwa wao wamejipanga kwa kuwa na wanasheria pamoja na wataalamu wa masuala ya uchumi ili kukabiliana na kesi hiyo na wanaamini mahakama ndiyo itatoa tafsiri ikiwa kwa kutoa takwimu hizo wamekosea kwani walichofanya wao ni uchambuzi wa takwimu zilizotolewa na Mamlaka husika.


Aidha amesema wanafikiria  kufungua kesi ya kutaka kuondoa vipengele vyote vya Sheria ya Takwimu nchini, vinavyozuia uhuru wa watu wengine kufanya uchambuzi na kutoa maoni yao juu taarifa hizo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search